Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Kambi ya maangamizi ya Auschwitz-Birkenau kusini mwa Poland
Unsplash/Jean Carlo Emer

Kamwe hatutowasahau wahanga wa mauaji ya maangamizi makubwa ya Holocaust: Guterres

Katika siku ya kimataifa ya kumbukumbu ya mauaji ya maangamizi makubwa ya Holocaust Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres, kupitia ujumbe maalum wa siku hii amesema " leo  tunawaomboleza watoto milioni 6 wa Kiyahudi, wanawake, na wanaume waliouawa katika mikono ya Manazi na washirika wao, na tunawaenzi Waroma na Wasinti, watu wenye ulemavu, na wengine wengi sana ambao waliteswa na kuuawa katika Maangamizi Makubwa ya Holocaust. 

Mahakama ya Kimataifa ya Haki ikisikiliza kessi ya Afrika Kusini dhidi ya Israel mjini The Hague. (Maktaba)
ICJ-CIJ/ Frank van Beek

ICJ yaitaka Israeli iepushe mauaji ya kimbari Gaza

Mahakama ya Kimataifa ya Haki, ICJ hii leo imeamua kuwa Israel lazima ichukue hatua zote za kuzuia vitendo vya mauaji ya kimbari katika mashambulizi yake dhidi ya wapalestina huko, Gaza, uamuzi unaofuatia shauri lililowasilishwa na Afrika Kusini la kutaka Mahakama hiyo ya Umoja wa Mataifa ichukue hatua za awali kwa mujibu wa Mkataba wa kimataifa wa kuepusha mauaji ya kimbari wa mwaka 1948. 

Sauti
2'13"
Aristote Muhawe ni mkimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC akiishi katika makazi ya wakimbizi ya Kyangwali magharibi mwa Uganda. Hapa anasoma shule ya sekondari pamoja na wakimbizi kutoka Sudan Kusini.
UN News

Elimu na Amani: Wakimbizi waelezea jinsi elimu ilivyobadili mtazamo wao hasi dhidi ya watu wengine

Nafasi ya elimu katika kuchagiza amani miongoni mwa wakimbizi na  jamii zinazowahifadhi imedhihirika huko Uganda wilayani Kikuube magharibi mwa nchi ambako kuna makazi ya wakimbizi ya Kyangwali. Hilo limethibitika wakati huu dunia kesho Januari 24 ikiadhimisha siku ya elimu duniani maudhui yakiwa kujifunza kwa ajili ya amani. 

Dkt. Venance Shillingi, Mhadhiri Mwandamizi kutoka Chuo Kikuu Mzumbe nchini Tanzania akizungumza na Idhaa ya Umoja wa Mataifa kando mwa mkutano wa UN na wanazuoni uliofanyika New York, kuanzia Desemba 5-7 2023.
UN/Assumpta Massoi

Ni kwa vipi mfumo wa wamasai kujikwamua unaweza kuwa mfano kwa wengine Afrika?

Kitendo cha kabila la jamii ya wamasai kuweza kujimudu na maisha hata baada ya ukame uliosababishwa na mabadiliko ya tabianchi kuvuruga upatikanaji wa malisho kwa ajili ya mifugo yao kimeonekana kama moja ya mbinu mujarabu zinazoweza kusaidia nchi za Afrika kujengea mnepo wananchi wapo pindi mbinu walizozoea kujipatia kipato zinapovurugika.

Malori yaliyosheheni msaada wa kibinadamu yakijiandaa kuingia Gaza kupitia kivuko cha Rafah
© UNICEF/Eyad El Baba

Mashirika ya UN yaomba kufunguliwe njia nyingine ya kufikisha misaada Gaza

Zikiwa ni zaidi ya siku 100 tangu kuibuka upya kwa mzozo huko Mashariki ya Kati, mashirika ya Umoja wa Mataifa hii leo yametoa taarifa inayoelezea kuongezeka kwa hatari ya baa la njaa na milipuko ya magonjwa ya kuambukiza huku yakisisitiza muarobaini pekee kwa sasa ni kuruhusu njia mpya za kuingiza misaada ya kwenda kutatua changamoto zinazowakabili wananchi walioko Gaza. 

Sauti
3'34"