Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Mwonekano wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa wakati wanachama wanapiga kura kuunga mkono rasimu ya azimio kuhusu hali ya Mashariki ya Kati tarehe 22 Desemba 2023.
UN Photo/Loey Felipe

Kura za Baraza la Usalama zapitisha Azimio zito kuhusu Gaza

Mchana huu wa Ijumaa 22 Novemba saa za New York, Marekani, Baraza la Usalama limeidhinisha azimio linalozitaka pande zinazohusika katika mzozo wa Gaza kuruhusu usambazaji wa haraka wa msaada wa kibinadamu kwa raia wa Palestina katika Ukanda wote wa Gaza. Nyaraka hiyo pia inataka hatua za haraka zichukuliwe ili kuunda mazingira ambayo yanasababisha usitishaji endelevu wa uhasama. Maandishi hayo yameidhinishwa kwa kura 13 za ndiyo, huku Marekani na Urusi zikijiepusha kupiga kura. 

 

Bukavu, Kivu Kusini. Uchaguzi wa Rais na wabunge umefanyika katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, 20 Desemba 2023.
MONUSCO/Michael Ali

DRC: Maisha yarejea hali ya kawaida huko Fataki, Ituri baada ya mashambulizi kutoka CODECO

Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC kazi ya kuhesabu kura inaendelea baada ya uchaguzi mkuu uliofanyika Jumatano na kuendelea katika baadhi ya maeneo jana Alhamisi, huku ikielezwa kwamba jimboni Ituri, maisha  yamerejea katika hali ya kawaida kwenye eneo la Fataki baada ya mwaka mmoja wa mashambulizi kutoka kwa wanamgambo waliojihami wa kundi la CODECO. 

Sauti
1'20"
Ngor Matiang, Mchezaji wa mpira wa Kikapu ambaye pia ni mwanafunzi kutoka Sudan Kusini.
UN News/Thelma Mwadzaya

Mpira wa kikapu unachangia amani, maendeleo na ustawi wa jamii

Kwa mara ya kwanza, Umoja wa Mataifa unaadhimisha siku maalum ya mpira wa kikapu ili kutambua mchango wake katika kuleta amani, maendeleo na ustawi wa jamii. Michezo, sanaa na mazoezi yana uwezo wa kubadili mitazamo, tabia, kadhalika kuhamasisha kuondoa vikwazo vya tofauti za rangi na siasa, kupambana na unyanyapaa na pia kumaliza ghasia. Kama michezo miengine ile, mpira wa kikapu unavuka mipaka yote, tamaduni na lugha. Ni kiunganishi kinachowaleta pamoja watu wa asili tofauti kutangamana, kujuana na hatimaye kuchangia kudumisha amani.

Upigaji kura wa kuchagua Rais na Wabunge huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC. Hapa ni Bukavu jimboni Kivu Kusini 20 Desemba 2023
MONUSCO Michael Ali

Uchaguzi DRC: Matokeo ya awali yaanza kubandikwa, wengine walipiga kura leo

Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, matokeo ya awali ya uchaguzi mkuu wa rais, magavana, wabunge na madiwani ambao ulifanyika jana, yameanza kubandikwa katika baadhi ya vituo huku maeneo mengine wapiga kura ambao  hawakuweza kupiga kura kutokana na sababu mbali mbali ikiwemo mvua na kuchelewa kuwasili kwa vifaa wameruhusiwa kupiga kura yao leo Alhamisi.