Sitisho la mapigano ndio njia pekee ya kumaliza 'jinamizi' Gaza- Guterres
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ameelezea matumaini yake kuwa azimio la kufanikisha upelekaji misaada zaidi ukanda wa Gaza lililopitishwa leo Ijumaa na Baraza la Usalama linaweza kufanikisha makubaliano ya sitisho la mapigano kati ya Israel na wanamgambo wa kipalestina, Hamas.