Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Husna Mbaraka, afisa msimamizi wa masuala ya ardhi, maliasili na jinsia wa FAO nchini Kenya akizungumza na Flora Nducha jijini New York Marekani.
UN News

Teknolojia inaleta tija kwa wanawake wakulima nchini Kenya: Husna- FAO

Shirika la chakula na kilimo la Umoja wa Mataifa FAO nchini Kenya linafanya kila juhudi kuhakikisha linatimiza wito wa Umoja wa Mataifa wa kutaka ubunifu na teknolojia vitumike kama nyenzo ya kumuinua mwanamke  kiuchumi na kijamii lakini pia katika utekelezaji wa malengo ya maendeleo endelevu SDGs na kuhakikisha hakuna anayesalia nyuma kwenye zama hizo za kidijitali.