Pamoja na changamoto za uhaba wa walimu na nyenzo za kufundishia, Uganda yadhamiria kukuza Kiswahili
Kuelekea maadhimisho ya pili ya siku ya lugha ya Kiswahili duniani julai 7 wananchi wa Uganda wanafanya kila juhudi kuhakikisha wanazungumza na kuelewa vyema lugha hiyo na kufuta usemi wa utani wa mitaani kuwa Kiswahili kimezaliwa Tanzania, kikafia Kenya na kuzikwa Uganda.