Sayansi yathibitisha kutwama kwa tabianchi; viongozi COP28 chukueni hatua
Dunia inazidi kuwa na joto kila uchao katika kasi isiyo ya kawaida, zinaonesha takwimumpya huku viongozi wanoakutana kwenye COP28 huko Dubai, Falme za Kiarabu kuanzia leo Alhamisi wakitakiwa kuchukua hatua kuondoa binadamu kwenye “tatizo kubwa” amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres.