Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Wajumbe wawasili katika mkutano wa COP28 kuhusu hatua za hali ya hewa.
© UNFCCC/Kiara Worth

HABARI KWA UFUPI

Mkutano wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabianchi COP28 umefungua pazia rasmi mjini Dubai katika Falme za nchi za Kiarabu kwa kuwaleta Pamoja wajumbe zaidi ya 60,000 kuangalia jinsi ya kuongeza hatua, fursa ya nyenzo za kujenga mnepo ikiwemo makubaliano ya kuanzishwa mfuko wa hasara na uharibifu ambayo yamepitishwa kwenye mkutano huo na pia kutumia ubunifu kudhibiti janga hilo.

Mabadiliko ya tabianchi yanachangia hali ya ukame katika maeneo mbalimbali duniani.
© WMO/Fouad Abdeladim

UDADAVUZI: COP28 ni nini, na kwa nini ni muhimu?

Hali ya joto duniani inaendelea kufikia viwango vya juu na kuvunja rekodi na, mwaka unavyofikia ukingoni, joto la kidiplomasia linaongezeka huku macho yote yakielekezwa Dubai, Falme za Kiarabu, ambako viongozi wa dunia wanakutana kuanzia tarehe 30 Novemba hadi 12 Desemba, ili kutathmini njia za kusonga mbele katika vita vya dunia dhidi ya mabadiliko tabianchi.

Kikundi Cha Bendera cha Pamoja cha Walinda Amani wa Tanzani na Nepali wakitoa Salamu kwa Mkuu wa kikosi cha Umoja wa Mataifa cha kulinda amani DRC, MONUSCO.
MONUSCO

Walinda amani wa MONUSCO kutoka nchini Tanzania na Nepal watunukiwa Nishani

Vikosi vya Walinda Amani kutoka Tanzania Kwa kushirikiana Walinda Amani wa Umoja wa Mataifa kutoka nchini Nepali wanaohudumu nchini Jamhuri ya Kidemkorasia ya Kongo – DRC wamefanya gwaride la pamoja na kutunikiwa Nishani za Umoja wa Mataifa na Mkuu wa kikosi cha Umoja wa Mataifa cha kulinda amani DRC, MONUSCO Luteni Jenerali Otavio Miranda Filho ikiwa ni kuthamini mchango wao wa kuhakikisha Amani ya Kudumu na Usalama vinapatikana nchini DRC.