Chonde chonde waachilieni watoto mliowateka Nigeria:UN
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametoa wito wa kuwaachilia mara moja na bila masharti mamia ya Watoto wavulana wanaoaminika kutekwa nyara na wanaodaiwa kuwa majambazi baada ya shambulio katika shule yao Kaskazini Magharibi mwa Nigeria.