Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Ukraine

UNDP inasaidia kutegua mabomu ya ardhini nchini Ukraine.
UNDP in Ukraine/Alexander Ratushnyak

Uondoaji wa mabomu ya kutengwa ardhini Ukraine ni mtihani na hatari kubwa: Paul Heslop

Umoja wa Mataifa umesema Ukraine sasa ni moja ya nchi zilizoathiriwa zaidi na mabomu ya kutegwa ardhini duniani huku ikadiriwa kwamba karibu thuluthi moja ya nchi hiyo imeghubikwa na vita eneo ambalo ukubwa wake ni mara nne na nusu ya nchi ya Uswisi. Umoja wa Mataifa umekuwa ukifanya kazi na serikali ya Ukraine kwa miaka 30 na umekuwa ukiongoza mpango wa utekelezaji wa uteguaji wa mabomu ya kutegwa ardhini tangu 2016. 

Sauti
2'33"
Mashirikak ya UN na wadau wake wanatoa misaada kwa watu walioathiriwa na mapigano mapya huko Lviv
© UNOCHA/Allaham Musab

UN yazindua ombi la dola bilioni 4.2 kwa ajili ya kuwasaidia Waukraine

Takriban miaka miwili sasa tangu majeshi ya Urusi yaanzishe "vita kamili na kuikalia Ukraine, amesema leo mkuu wa Umoja wa Mataifa wa misaada ya kibinadamu na masuala ya dharura Martin Griffiths akitoa ombi la dharura la pamoja na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR la dola bilioni 4.2 ili kuwasaidia walio hatarini nchini Ukraine.

Olga (kushoto) akiwa na mbwa na mtoto wake, waathirika wa vita inayoendelea nchini Ukraine.
UNHCR Video

Bila UNHCR sijui ningekaa wapi: Olga muathirika wa vita Ukraine

Kutana na Olga mwathirika wa vita inayoendelea nchini Ukraine ambaye baada ya nyumba yake kushambuliwa na kombora mjini Borodyanka alikataa tamaa ya Maisha lakini sasa mradi wa UNHCR wa kukarabati nyumba zilizoharibiwa na vita Ukraine umemfufulia matumaini ya Maisha yeye na mwanaye “Katika maisha mambo hayawezi kuwa mteremko tu, kuna wakati unapitia magumu na ukiwa na uvumilivu utayashinda.

Sauti
3'9"