Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Ukraine

Mkuu wa ofisi ya Umoja wa Mataifa ya  kuratibu misaada ya dharura, OCHA, Martin Griffiths akiwa Kherson katika ziara yake ya siku nne nchini Ukraine.
© UNOCHA/Saviano Abreu

Umeme, mabomu ya kutengwa ardhini na uchumi vipewe kipaumbele Ukraine: Griffiths

Mkuu wa ofisi ya Umoja wa Mataifa ya  kuratibu misaada ya dharura, OCHA, Martin Griffiths amehitimisha ziara yake ya siku nne nchini Ukraine na kutaja mambo makuu matatu muhimu ya kupatiwa kipaumbele kuwa ni mosi; kurejesha umeme kwenye makazi, pili kutegua mabomu yaliyoko kwenye makazi ya watu na tatu, ni kuchechemua shughuli za kiuchumi ili maisha yaweze kuendelea na kwamba Umoja wa Mataifa uko tayari kusaidia.  

Meli ya kwanza ya kibiashara ikiwa na nafaka kupitia mpango wa usafirishaji wa nafaka kupitia Bahari Nyeusi
© UNOCHA/Levent Kulu

UN yaingiwa hofu kufuatia Urusi kusitisha ushiriki wake kwenye makubaliano ya usafirishaji nafaka Bahari Nyeusi

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres ameelezea wasiwasi wake mkubwa juu ya uamuzi wa Urusi kusitisha ushiriki wake kwenye makubaliano ya usafirishaji nafaka kupitia Bahari Nyeusi, au kwa kiingereza, Black Sea Grain Initiative, makubaliano ambayo yalianzishwa tarehe 22 mwezi Julai mwaka huu ili kuwezesha Ukraine kuanza kuuza tena nje ya nchi hiyo vyakula na mbolea.

Watoto wakimbizi kutoka Somalia wakiwa kwenye kambi ya wakimbizi ya Daadab nchini Kenya ambako WFP inawapatia misaada ya dharura.
WFP/Rose Ogola

Majanga yanavyozidi kushamiri isiwe kisingizio cha kusigina haki za mtoto- UN

Wataalamu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa hususan zile za mtoto wametoa taarifa ya pamoja hii leo huko Geneva, Uswisi wakisema  majanga ya kiafya, kibinadamu na yale  yanayohusiana na tabianchi yakizidi kuongeza changamoto kubwa duniani kila uchao kama vile ukimbizi wa ndani, ukatili wa kingono na njaa, serikali lazima zikumbuke kuwa watoto wana haki kamilifu za kimsingi za kibinadamu na kwamba haki hizo zinapaswa kulindwa.