Dunia inashuhudia mgogoro wa kihistoria wa chakula huku njaa ikibisha hodi katika milango mingi: OCHA
Mratibu wa umoja wa Mataifa wa masuala ya kibinadamu na misaada ya dharura Martin Griffiths amesema masuala ya kibinadamu duniani yanakabiliwa na mtihani mkubwa ambao haujawahi kushuhudiwa huku mahitaji yakiongezeka kila uchao duniani kote, migogoro ikipandiana na mamilioni ya watu wakihitaji msaada.