Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Ukraine

Mkurugenzi Mkuu wa IAEA Rafael Gross (kulia) akikutana na Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky mjini Kyiv.
Ikulu ya Ukraine

IAEA yapanua wigo wa shughuli zake Ukraine

Mkurugenzi Mkuu wa shirka la Umoja wa Mataifa la nishati ya atomiki, IAEA, Rafael Mariano Grossi amemfahamisha Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky mjini Kyiv kuhusu upanuzi wa wigo wa shughuli za shirika hilo nchini humo ili kuisaidia kuhakikisha ulinzi na usalama wa nyuklia katika kinu chake wakati huu ambapo operesheni na mashambulizi ya kijeshi yanaendelea kutoka Urusi.

Ukosefu wa usalama unazidi kushamiri nchini Haiti
JOA/Yes Communication Design

Uvunjaji wa sheria umetapakaa duniani, tuchukue hatua sasa- Katibu Mkuu UN

Hii leo Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limekuwa na mjadala wa wazi kuhusu utawala wa sheria ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa Matifa Antonio Guterres amesema ingawa nchi wanachama, mashirika ya kikanda, ya kiraia na sekta binafsi wana wajibu wa kuchangia katika kujenga na kulinda utawala wa sheria, hali ilivyo hivi sasa ni tofauti na kinachoonekana bado kuna safari ndefu ya kufikia lengo la utawala wa sheria.  

Kwa wakulima wa Ukraine, vita vinavyoendelea vinamaanisha kutokuwa na uwezo wa kuuza nje mazao yao, na matarajio mabaya ya mavuno yao kuharibika katika banda.
© UNOCHA/Matteo Minasi

EU-FAO kuhakikisha ahueni na maendeleo ya minyororo ya thamani ya kilimo Ukraine

Kaya za vijijini, wakulima wadogo na wafanyabiashara wadogo wa kilimo nchini Ukraine watanufaika na mradi wa dola milioni 15.5 unaofadhiliwa na Muungano  wa Ulaya (EU) na kutekelezwa na shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na Kilimo (FAO) ili kusaidia utendakazi, uifuatiliaji na uimarishaji wa minyororo ya thamani katika kilimo, uvuvi na sekta ya misitu, na kukabiliana na hali ya wakati wa vita.

Mkuu wa ofisi ya Umoja wa Mataifa ya  kuratibu misaada ya dharura, OCHA, Martin Griffiths akiwa Kherson katika ziara yake ya siku nne nchini Ukraine.
© UNOCHA/Saviano Abreu

Umeme, mabomu ya kutengwa ardhini na uchumi vipewe kipaumbele Ukraine: Griffiths

Mkuu wa ofisi ya Umoja wa Mataifa ya  kuratibu misaada ya dharura, OCHA, Martin Griffiths amehitimisha ziara yake ya siku nne nchini Ukraine na kutaja mambo makuu matatu muhimu ya kupatiwa kipaumbele kuwa ni mosi; kurejesha umeme kwenye makazi, pili kutegua mabomu yaliyoko kwenye makazi ya watu na tatu, ni kuchechemua shughuli za kiuchumi ili maisha yaweze kuendelea na kwamba Umoja wa Mataifa uko tayari kusaidia.