Aleppo ni kisawe cha Jehanam, na jamii ya kimataifa imeshindwa- Ban
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon leo amefanya mkutano rasmi wa mwisho na waandishi wa habari mjini New York ikiwa ni takribani majuma mawili kabla ya kumaliza awamu ya pili na ya mwisho ya uongozi wake katika chombo hicho .