Neno la wiki- Mazishi au maziko?
Ijumaa ya tarehe 29 Mei mwaka 2016 tuliangazia matumizi ya maneno maziko na mazishi. Mtaalamu wetu alikuwa Onni Sigalla, mhariri mwandamizi, Baraza la Kiswahili la Taifa, BAKITA, huko nchini Tanzania.
Ijumaa ya tarehe 29 Mei mwaka 2016 tuliangazia matumizi ya maneno maziko na mazishi. Mtaalamu wetu alikuwa Onni Sigalla, mhariri mwandamizi, Baraza la Kiswahili la Taifa, BAKITA, huko nchini Tanzania.
Kamati ya kupinga ubaguzi wa rangi imehitimisha Ijumaa hii ripoti ya pamoja ya Rwanda kuhusu utekelezaji wake wa makubaliano ya kimataifa ya kupinga aina zote za ubaguzi wa rangi.
Tarehe 25 mwezi Aprili ya kila mwaka, dunia huadhimisha siku ya malaria, msisistizo ukiwa kutokomeza ugonjwa huo. Kwa mujibu wa takwimu za shirika la afya ulimwenguniWHO, takribani watu bilioni 3.2 ambayo ni karibu nusu ya idadi ya watu duniani wako katika hatari ya kuambikizwa malaria.
Watu milioni 1.4 katika mikoa 18 nchini Angola wameathiriwa na ukame mkubwa uliosababishwa na hali ya hewa ya El Niño nchini humo, wakihitaji usaidizi wa kibinadamu, kwa mujibu wa ofisi ya Mratibu Mkaazi wa Ofisi ya kuratibu masuala ya kibinadamu nchini humo (OCHA).
Kongamano la 66 la Idara ya Habari ya Umoja wa Mataifa na Mashirika yasiyo ya kiserikali (NGOs) litafanyika mjini Gyeongju, Korea Kusini, kuanzia Mei 30 hadi Juni mosi, 2016, na tayari maandalizi yameanza.
Mji wa Kenya wa Kisumu unaongoza mashiniani katika kutekeleza makubaliano ya Sendai ya kupunguza majanga barani Afrika katika juhudi za kutafuta suluhu endelevu kukabiliana na changamoto ya ukauji wa miji na mabadiliko ya tabianchi.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon, amekaribisha uteuzi wa mawaziri wa serikali ya mpito nchini Sudan Kusini, kulingana na makubaliano ya Agosti 17 2015 ya kuutanzua mgogoro nchini humo.
Mpango wa Umoja wa mataifa nchini Iraq UNAMI, umeelezewa hofu yake dhidi ya uamuzi wa tume ya mawasiliano na vyombo vya habari nchini Iraq kutoa amri ya kufunga ofisi za kituo cha Al Jazeera mjini Baghdad.
Mzozo Ukraine ukiingia mwaka wa tatu, baraza la usalama la Umoja wa Mataifa limeelezwa kuwa hali ya kibinadamu inazidi kuzorota na kutia wasiwasi mkubwa.
Mtaalam maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu haki za watu wenye ulemavu, Catalina Devandas, amesema kuwa kuna fursa nzuri ya kutimiza haki za watu wenye ulemavu nchini Zambia, na kutoa wito kwa serikali ya nchi hiyo itekeleze kikamilifu baadhi ya sera na mikakati yake mizuri.