Baraza Kuu launda chombo kuchagiza uchunguzi wa haki Syria
Baraza kuu la Umoja wa Mataifa limepitisha azimio linalounda utaratibu wa kusaidia kuchunguza ukiukwaji wa haki za binadamu ikiwemo uhalifu wa kivita tangu kuanza kwa mzozo nchini Syria mwaka 2011. Azimio hilo lilipitishwa kwa kura 105 nchi 15 zikipinga ilihali 52 hazikupiga kura.