Macho ya dunia yalielekezwa Glasgow, Scotland, wakati mkutano wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabianchi unaojulikana kama COP26 ukifunguliwa tarehe 31 Oktoba, huku wanadiplomasia na wanasiasa wa Umoja wa Mataifa wakitafuta ahadi mpya za kuzuia utoaji wa gesi chafuzi na kukabiliana na athari za kuongezeka joto kwenye sayari
COP26 inafanyika katika kampus ya matukio Scotland, eneo hili maalum lilishinda tuzo ya eneo la utalii linalolinda mazingira katikati mwa Glasgow. Eneo hili lIna nafasi tano za mikutano zilizounganishwa, zinazotambulika zaidi kama zinavyoonekana kwenye picha hii iliyopigwa wakati jua linapotua, wanja maarufu wa OVO Hydro una uwezo wakuchukua watu 14,000.
COP26 imekuwa moja ya Mikutano maarufu ya mabadiliko ya tabianchi ya Umoja wa Mataifa katika historia, na takriban watu 50,000 wamejiandikisha kushiriki mtandaoni na nje ya mtandao. Pichani hapa ni misururu mirefu ya washiriki wakisubiri kupita sehemu ya ulinzi na kuingia eneo liitwalo ‘Blue Zone’ kwenye Kampasi ya Tukio ya Scotland, ambako mikutano mingi inafanyika.
Mkutano huu wa Viongozi wa Dunia ulihudhuriwa na Wakuu wa Nchi na Serikali wapatao 120. Mbali kuonekana katika taa za jukwaani, viongozi wengi walitangamana nyuma ya pazia. Hapa, Kansela wa Ujerumani Angela Merkel (kushoto), Mia Motley, Waziri Mkuu wa Barbados, (Katikati) na Sheikh Hasina, Waziri Mkuu wa Bangladesh (kulia), wanaonekana wakipiga soga pamoja kabla ya tukio kuu.
Wakati Mkutano wa Viongozi wa Dunia wa COP26 ukiendelea, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres aliwaambia viongozi 120 huko Glasgow: "Tunakabiliwa na chaguo kali. Ama tuzuie [mabadiliko ya tabianchi] - au yatuzuie”.
Mashirika ya kiraia yamekuwa yakishiriki kikamilifu wakati huu wa COP, na maandamano ya kila siku ya kudai haki ya mabadiliko ya tabianchi. Hapa, kikundi kilicho beba mabango kinajitokeza kwa wapiga picha kwenye eneo la mkutano ukanda wa Eneo la Bluu.
Watu mashuhuri pia walifika kwenye Mkutano wa Viongozi wa Dunia. Hapa, mwigizaji mashuhuri na mwanaharakati wa mazingira Leonardo DiCaprio akiwa kwenye mazungumzo ya moja kwa moja na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres.
Pia kulikuwa na hatua nje ya ukumbi kuu, huku maelfu ya waandamanaji wakikusanyika katikati mwa Glasgow kudai hatua za hali ya hewa. Dinosaur ‘T- Rexscilient’ alisafiri umbali wote kutoka Bolivia ili kushiriki katika maandamano ya vijana yaliyoongozwa na mwanaharakati wa Uswidi Greta Thunberg.
Wahudhuriaji katika COP26 wamekuwa wakining'inia vipandikizi vya umbo la majani ya rangi kwenye ukumbi huo. Kila moja imeandikwa "ahadi" kwa viongozi wa ulimwengu. Katika picha hii, mshiriki amewataka kuahidi kuwa watatunga sheria ya kupunguza utoaji wa gesi chafu, ambayo ni moja ya malengo makuu ya COP26.