Daktari Marie-Roseline Bélizaire, mtaalamu wa magonjwa ya mlipuko kutoka Haiti ambaye ameshiriki katika harakati dhidi ya milipuko ya magonjwa barani Afrika ikiwemo ugonjwa wa Ebola. Hivi sasa yuko katika Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR ambako anasaidia wat kukabiliana na virusi hatari vya Corona.
Debryna Dewi Lumanauw, mtafiti msomi katika tiba za dharura, alifanya kazi na moja ya timu za kwanza za matibabu kupelekwa katika hospitali ya huduma za dharura ya COVID-19 huko Jakarta, Indonesia.
Kila siku alienda katika eneo la wagonjwa mahututi. Anasema limekuwa ni sawa na janga kubwa ambalo hajawahi kushuhudia.
Mtengeneza filamu na mwanaharakati wa kutetea haki za kibinadamu Hassan Akkad (aliye majini upande wa kushoto) alikimbia mzozo nchini mwake Syria miaka minne iliyopita.
Aliokolewa kutoka Bahari ya Aegean na akapata hifadhi salama huko Uingereza.
Ana nia nzuri na moyo wa kusaidia wakati huu wa mlipuko wa COVID-19, kwa hivyo alijiunga na timu ya wasafishaji wanaotakasa wodi za wagonjwa kwenye hospitali moja jijini London.
Daktari Edna Patricia Gomez alikimbia Venezuela mwaka 2018 na sasa anafanya kazi nchini Colombia ya kutoa huduma za afya kwa wanawake wakimbizi kutoka Venezuela nchini Colombia. Wakati virusi vya Corona vilipoenea, alianza kusaidia uchunguzi wa virusi hivyo vya Corona na utoaji wa matibabu.
Nchini Venezuela, Belitza Bermudez (kulia) anafanya kazi ya afisa wa ulinzi katika mji ulioko mpakani.Yeye hupokea maelfu ya waliorejeshwa kutokana na zuio la kuingia kwa sababu ya COVID-19 hivyo anahakikisha waliorejea wanaenda karantini kwa siku zinazostahili punde wanapofika.
Shadi Mohammedali (katikati nyuma) ni mkimbizi kutoka Ukanda wa Gaza ambaye sasa anafanya kazi katika kambi ya wakimbizi nchini Ugiriki. Jukumu lake ni kusaidia watu kupata ufahamu kuhusu jinsi ya kujikinga na COVID-19. Akiwa ni mtu ambaye hivi karibuni alikuwa katika hali kama hiyo, anaelewa jinsi wakimbizi walioko kambini wanahisi."Mtu alinisaidia; sasa ni zamu yangu kulipa. "
Mashujaa halisi wa maisha wanatambuliwa Siku ya Utu wa Kibinadamu Duniani ambayo huadhimishwa kila mwaka mnamo tarehe 19 mwezi Agosti.