Walinda amani wa UN wamepelekwa nchini Haiti kwa miaka 15 iliyopita kufuatia kuyumba kwa uatawala wa kishera, na mpango huo unakamilika Oktoba mwaka huu wa 2019. Mwanzoni, mnamo mwaka wa 2005, wanajeshi, polisi na walinda amani raia walihamia kwenye kisiwa hicho cha Karibea kama jukumu lao la kulinda raia na kusaidia kurejesha utawala wa seheria na utulivu.
Mpango wa UN pia ulifanya kazi na jamii kwenye miradi ya kupunguza machafuko. Walinda amani waliunga mkono wafanyikazi hawa wa Haiti, wakiwasaidia kujenga kuta na kupanda miti ili kuhifadhi mazingira na kuzuia mafuriko. Mradi huo pia uliwezesha fursa za kiuchumi na kijamii kwa washiriki wa zamani wa magenge ya uhalifu.
Mpango wa sasa wa kulinda amani ya Umoja wa Mataifa unafungwa Oktoba 15, mwaka huu wa 2019 na utabadilishwa na nafasi yake kuchukuliwa na mpango wa kisiasa, ukiendeleza maendeleo ambayo yamefanywa na mamlaka ya Haiti ya kuimarisha utulivu, usalama, utawala, pamoja na sheria na haki za binadamu.