Hivi sasa kuna karibu maafisa wa polisi 11,000 wa Umoja wa Mataifa kutoka nchi 88 wanaohudumu kwenye operesheni za ulinzi wa amani. Asilimia 21 waliotumwa nan chi wachangiaji wa vikosi ni wanawake . Huyu ni afisa kutoka Indonesia akifanya ukaguzi katika kambi ya wakimbizi wa ndani nchini Sudan Kusini.
Katika makao Makuu ya Umoja wa Mataifa New York , Maafisa wa polisi wa Umoja wa Mataifa (UNPOL) walikusanyika kujadili jukumu muhimu la wanawake maafisa wa polisi katika operesheni za Umoja wa Mataifa kote duniani na joinsi gani ya kuongeza idadi yao kwenye operesheni hizo.
Wanawake maafisa wa poolisi wa Umoja wa Mataifa wanaweza kuwa kiungo muhimu baina ya mpango wa ulinzi wa amani na wenyeji, hususan wanawake ambao kwa sababu ya mila na desturi itakuwa vigumu kushirikiana kwa karibu na wanaume kama ilivyo Darfur ambako mpango wa pamoja wa Muungano wa Afrika na Umoja wa Mataifa UNAMID upo.
Nchini Sudan Kusini , maafisa wa polisi wananwake wanaohudumu katika mpango wa UNMISS mara kwa mara wanakuwa karibu na wanawake waliotawanywa na machafuko ya takriban miaka mitano ya vita vya wenyewe kwa wenyewe. Mahusiano hayo yanaweza kuwawezesha watu wa jamii hiyo kuelewa haki zao na kupata fursa ya huduma.
Maafisa wa polisi wanatumwa nan chi zao kufanya kazi maalumu , lakini pia wanawasili kikosi , kinachojulikana kama kikosi maalumu cha polisi kilichoundwa au FPU’s. Nchini Sudan Kusini karibu nusu ya kikosi maalum cha maafisa wa polisi kutoka Rwanda ni wanawake. Kimataifa idadi yao katika operesheni za ulinzi wa Amani ni asilimia 7 tu.
Hivi sasa kuna wanawake wawili tu ambao ni malkamishina wa polisi katika operesheni 14 za Umoja wa Mataifa kote duniani. Unamisi Vuniwaqa kutoka Fiji ndiye mkuu wa operesheni za polisi kwenye mpango wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini, UNMISS.