![Wakazi wa Yambio wakiendelea na shughuli zao kwenye eneo la soko Wakazi wa Yambio wakiendelea na shughuli zao kwenye eneo la soko](https://global.unitednations.entermediadb.net/assets/mediadb/services/module/asset/downloads/preset/assets/2018/08/02-08-2018-Market-Yambio-activity.jpg/image770x420cropped.jpg)
Siku ya soko wanawake kwa wanaume wanajitokeza kwa ajili ya kuuza na kununua bidhaa. Pichani mwanamke akiwa na mwanae na kando ni madumu ya maji ambapo atatumia fursa hiyo pia kuhakikisha akirudi nyumbani, anarejea na maji ambayo ni moja ya rasilimali adimu nchiin Sudan Kusini kutokana na vita vya wenyewe kwa wenyewe vinavyoendelea.
![Wachuuzi wa mboga kwenye soko Yambio jimbo la Gbudue nchini Sudan Kusini Wachuuzi wa mboga kwenye soko Yambio jimbo la Gbudue nchini Sudan Kusini](https://global.unitednations.entermediadb.net/assets/mediadb/services/module/asset/downloads/preset/assets/2018/08/02-08-2018-Market-Yambio-sellers.jpg/image770x420cropped.jpg)
Uchuuzi wa mboga za majani ukiendelea kwenye moja ya majengo yaliyopo katika soko la mjini Yambio, jimboni Gbudue, kusini-mashariki mwa Sudan Kusini. Kupitia biashara hii ya mboga za majani, wachuuzi hawa wanawake wanajipatia kipato cha kuwawezesha kununua mahitaji mengine muhimu ya familia zao. Umoja wa Mataifa kupitia ujumbe wake wa kulinda amani Sudan Kusini unahakikisha unafanya doria kwenye maeneo ya raia ili amani iwepo na wananchi waweze kuendelea na shughuli zao bila woga.
![Kijana akimpaka rangi ya kucha mteja wake kwenye eneo la soko mjini Yambio Kijana akimpaka rangi ya kucha mteja wake kwenye eneo la soko mjini Yambio](https://global.unitednations.entermediadb.net/assets/mediadb/services/module/asset/downloads/preset/assets/2018/08/02-08-2018-Market-Yambio-women.jpg/image770x420cropped.jpg)
Huduma za urembo nazo zinapatikana katika soko la Yambio jimboni Gbudue nchini Sudan Kusini ambapo pichani ni kijana ambaye anafanya kazi ya kupaka rangi za kucha, akimhudumia mteja wake. Doria zinazofanywa na walinda amani wa Umoja wa Mataifa zimewezesha wafanyabaishara na wananchi nao kuendelea na shughuli zao.
![Huduma za intaneti nazo zinapatikana sokoni Yambio ambapo vijana wanapata fursa ya kurambaza wavuti mbalimbali ili kupata taarifa Huduma za intaneti nazo zinapatikana sokoni Yambio ambapo vijana wanapata fursa ya kurambaza wavuti mbalimbali ili kupata taarifa](https://global.unitednations.entermediadb.net/assets/mediadb/services/module/asset/downloads/preset/assets/2018/08/02-08-2018-Market-Yambio-youth.jpg/image770x420cropped.jpg)
Na kwa vijana nao ambao wanapenda kufuatilia kile kinachoendelea pande mbalimbali duniani, kuna vioski vinavyotoa huduma za intaneti kama inavyoonyesha pichani ambapo vijana wamesaka huduma hiyo kwenye moja ya vioski sokoni Yambio jimboni Gbudue nchini Sudan Kusini.