Siku ya soko wanawake kwa wanaume wanajitokeza kwa ajili ya kuuza na kununua bidhaa. Pichani mwanamke akiwa na mwanae na kando ni madumu ya maji ambapo atatumia fursa hiyo pia kuhakikisha akirudi nyumbani, anarejea na maji ambayo ni moja ya rasilimali adimu nchiin Sudan Kusini kutokana na vita vya wenyewe kwa wenyewe vinavyoendelea.
Uchuuzi wa mboga za majani ukiendelea kwenye moja ya majengo yaliyopo katika soko la mjini Yambio, jimboni Gbudue, kusini-mashariki mwa Sudan Kusini. Kupitia biashara hii ya mboga za majani, wachuuzi hawa wanawake wanajipatia kipato cha kuwawezesha kununua mahitaji mengine muhimu ya familia zao. Umoja wa Mataifa kupitia ujumbe wake wa kulinda amani Sudan Kusini unahakikisha unafanya doria kwenye maeneo ya raia ili amani iwepo na wananchi waweze kuendelea na shughuli zao bila woga.
Huduma za urembo nazo zinapatikana katika soko la Yambio jimboni Gbudue nchini Sudan Kusini ambapo pichani ni kijana ambaye anafanya kazi ya kupaka rangi za kucha, akimhudumia mteja wake. Doria zinazofanywa na walinda amani wa Umoja wa Mataifa zimewezesha wafanyabaishara na wananchi nao kuendelea na shughuli zao.
Na kwa vijana nao ambao wanapenda kufuatilia kile kinachoendelea pande mbalimbali duniani, kuna vioski vinavyotoa huduma za intaneti kama inavyoonyesha pichani ambapo vijana wamesaka huduma hiyo kwenye moja ya vioski sokoni Yambio jimboni Gbudue nchini Sudan Kusini.