2003: Wapiganaji wa zamani wakiwasilisha silaha kwenye kambi ya Schieffelin, nje yam ji mkuu Monrovia, wakati wa kampeni ya upokonyaji silaha. Wakati wa operesheni nzima ya ulinzi wa amani Umoja wa Mataifa uliwapokonya silaha zaidi ya wapiganaji 100,000 na kukusanya silaha zaidi ya 21,000. Picha:UN/Astrid-Helene Meister
2005: Wapiga kura wa Liberia mjini Doe wakiwa wamepanga foleni katikati ya dimbwi la maji wakisubiri kupiga kura katika uchaguzi wa kwanza wa kidemokrasia tangu kumalizika vita vya wenyewe kwa wenyewe. Ellen Johnson Sirleaf alishinda uchaguzi huo baada ya kuru za duru ya pili na kuwa mwanamke wa kwanza kuchaguliwa kidemokrasia kuwa Rais barani Afrika. Picha :UN/Eric Kanalstein
2007: Kikosi cha India kwenye mpango wa Amani wa Umoja wa Mataifa kikijumuisha zaidi wanawake, kikibadilisha kofia zao na kuchukua kofia za blu za Umoja wa Mataifa, kilipowasili Monrovia kuanza kazi ya ulinzi wa amani. Idadi kubwa ya walinda Amani wanawake iliwachagiza wanawake Liberia kujiunga na sekta ya ulinzi ikiwemo jeshi la polisi la taifa. Picha: UN/Eric Kanalstein