Mfungwa aliyehukumiwa kwa uhalifu wa mauaji ya kimbari dhidi ya Watutsi akionyesha barua yake ya kukiri makosa na kuomba msamaha baada ya kupata mafunzi ya maridhiano ya kijamii yanayotolewa na magereza kwa msaada wa UNDP Rwanda, huko Rwamagana.
Mwakilishi wa taasisi ya fedha akimpa mafunzo mkimbizi mjasiriamali ya jinsi ya kutumia akaunti yake ya benki kwa kutumia simu ya rununu kama sehemu ya mradi wa UNCDF nchini Rwanda wa ujumuishwaji wa kidijitali katika masuala ya fedha.
Katika ulinzi wa amani: Kampeni ya uelimishaji dhidi ya COVID-19 nchini Sudan Kusini kupitia (UNMISS). Walinda amani wanawake kutoka Rwanda wakiwafundisha wanafunzi wa shule ya msingi ya Kapuri jinsi ya kuvaa barakoa.
WFP inaisaidia serikali ya Rwanda kutekeleza program yam lo shuleni kwa kutumia vyakula vinavyolimwa nchini humo, ikiunganisha elimu, afya, lishe na kilimo.