Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UN News

Makala Maalum

Ukuaji wa Kiuchumi Azimio la 5 la Manama limepitishwa hii leo huko Manama, mji mkuu wa Bahrain na washiriki wa Jukwaa la Kimataifa la Uwekezaji kwa Wajasiriamali likiwa na wito wa pamoja na mambo mengine  likisihi jamii ya kimataifa na wadau wote katika sekta ya umma na binafsi kutumia nguvu ya ujasiriamali na uwekezaji katika nyanja zote za kiuchumi na kijamii kama kitovu cha kufanikisha Malengo ya Maendeleo Endelevu, SDGs kwa kupatia kipaumbele makundi maalum wakiwemo watu wenye ulemavu, wanawake, vijana na familia zinazohaha kutumia uwezo wa kuzalisha ili kujikimu kimaisha.

Habari Nyinginezo

Malengo ya Maendeleo Endelevu Suala la kuwekeza kwa wanawake wajasiriamali kwenye maeneo yenye mizozo duniani limepatiwa uzito hii leo mwishoni mwa mkutano wa 5 wa Umoja wa Mataifa kuhusu uwekezaji kwa wajasiriamali, WEIF 2024 huko Manama, mji mkuu wa Bahrain, jukwaa lililoratibiwa na Umoja wa Mataifa na wadau wake.
Ukuaji wa Kiuchumi Ripoti ya Umoja wa Mataifa ya katikati ya mwaka ya hali na mtazamo wa uchumi wa Dunia kwa mwaka 2024 iliyotolewa leo inaonyesha matarajio ya kiuchumi duniani yameboreka tangu utabiri uliotolewa Januari 2024, lakini mtazamo ni wa matumaini yanayohitaji tahadhari.