Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

UNFPA na wadau waendelea kutoa baadhi ya huduma za kuokoa maisha kwa wanawake wajawazito
© PMRS Gaza

Gaza: Huku wanakimbia vita wanawake wa Gaza inakuwaje wakiwa katika hedhi?

Kunapozuka mizozo na machafuko wananchi wote wanaathirika kwasababu maisha yao yanaparanganyika kabisa tofauti na walivyokuwa wamezoea. Watoto waliokuwa wakienda shule sasa hawaendi, si wafanyabiashara, wakulima wala viongozi wa dini wanaotekeleza majukumu yao ya kila siku na suala moja lililo kweli kwa kila mtu ni kuwa wanatafuta kila namna ya kuokoa maisha yao na wengi njia hiyo huwa ni kukusanya virango vyao kidogo wanavyoweza kubeba na kukimbia kuokoa nafsi zao. 

Baraza la Usalama la UN lilipokutana leo 5 Februari 2024 kujadili tishio la amani na usalama Mashariki ya Kati
UN /Evan Schneider

Baraza la Usalama lakutana kujadili mashambulizi ya Marekani huko Syria na Iraq

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa Jumatatu alasiri limekuwa na kikao cha dharura kufuatia ombi la Urusi, wakati huu ambao vita huko Gaza inaendelea kuchochea mivutano huko Mashariki ya Kati, hasa uwezekano wa kuathiri vibaya amani na usalama kwenye ukanda huo. Mkuu wa Idara ya UN ya Masuala ya Kisiasa, ameliomba Baraza lizuie kushamiri zaidi kwa uhasama na mivutano  kwenye ukanda mzima

Uvutaji wa tumbaku unaunaathiri afya yako.
© Unsplash/Andres Siimon

Nilivuta sigara tangu mtoto, acheni haina maana- Thierry

Nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR, simulizi ya mtu aliyeanza kuvuta sigara akiwa kijana balehe na sasa ameamua kuacha inamulika ni kwa nini shirika la Umoja wa Mataifa la afya duniani, WHO linasisitiza umuhimu wa kampeni za kuacha tumbaku kwani ni miongoni mwa visababishi vikubwa vya maambukizi ya saratani ya mapafu inayooongoza kwa kuua zaidi vifo miongoni mwa wanaume duniani. 

Sauti
2'26"
Ujenzi wa madarasa nchini Mozambique yanayohimili hali mbaya za hewa ikiwemo vimbunga vinavyong’oa mapaa.
UN Habitat Mozambique

Iwe mvua iwe upepo mkali madarasa yetu ni salama: Mwanafunzi Msumbiji

Kila mwaka, Msumbiji hukabiliwa na matukio ya hali mbaya za hewa kupindukia kama vile vimbunga na mafuriko, matukio ambayo husababisha uharibifu wa shule na hatimaye watoto kushindwa kujifunza. Hata hivyo, ujenzi wa madarasa yanayohimili matukio kama vile pepo kali na mafuriko umeleta nuru na matumiani kwa watoto, wazazi na walimu. Madarasa haya yanawezesha watoto kubakia salama hata wakati wa mvua na upepo mkali. Hali hii ni uwekezaji wa kudumu kwani ni  hakikisho kwa watoto kuendelea kupata elimu na mustakabali wao kuwa bora. 

Sauti
4'11"
Wapalestina wakiwa kwenye foleni ya kutafuta chakula kwenye mvua kwenye makazi huko Deir Al-Balah, Gaza.
© UNRWA

Mgogoro wa ufadhili UNWRA ukiendelea raia Gaza wapekua malori kusaka mlo

Wakati Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres leo ankukutana na wawakilishi kutoka nchi zinazotoa misaada kwa shirika la Umoja wa Mataifa la msaada kwa wakimbizi wa Kipalestina UNRWA kufuatia madai ya baadhi ya wafanyakazi wa shirika hilo kushirikiana na Hamas, shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO, leo limesema sasa si wakati wa kuwatelekeza watu wa Gaza.

Kambi ya maangamizi ya Auschwitz-Birkenau kusini mwa Poland
Unsplash/Jean Carlo Emer

Kamwe hatutowasahau wahanga wa mauaji ya maangamizi makubwa ya Holocaust: Guterres

Katika siku ya kimataifa ya kumbukumbu ya mauaji ya maangamizi makubwa ya Holocaust Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres, kupitia ujumbe maalum wa siku hii amesema " leo  tunawaomboleza watoto milioni 6 wa Kiyahudi, wanawake, na wanaume waliouawa katika mikono ya Manazi na washirika wao, na tunawaenzi Waroma na Wasinti, watu wenye ulemavu, na wengine wengi sana ambao waliteswa na kuuawa katika Maangamizi Makubwa ya Holocaust. 

Mahakama ya Kimataifa ya Haki ikisikiliza kessi ya Afrika Kusini dhidi ya Israel mjini The Hague. (Maktaba)
ICJ-CIJ/ Frank van Beek

ICJ yaitaka Israeli iepushe mauaji ya kimbari Gaza

Mahakama ya Kimataifa ya Haki, ICJ hii leo imeamua kuwa Israel lazima ichukue hatua zote za kuzuia vitendo vya mauaji ya kimbari katika mashambulizi yake dhidi ya wapalestina huko, Gaza, uamuzi unaofuatia shauri lililowasilishwa na Afrika Kusini la kutaka Mahakama hiyo ya Umoja wa Mataifa ichukue hatua za awali kwa mujibu wa Mkataba wa kimataifa wa kuepusha mauaji ya kimbari wa mwaka 1948. 

Sauti
2'13"
Aristote Muhawe ni mkimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC akiishi katika makazi ya wakimbizi ya Kyangwali magharibi mwa Uganda. Hapa anasoma shule ya sekondari pamoja na wakimbizi kutoka Sudan Kusini.
UN News

Elimu na Amani: Wakimbizi waelezea jinsi elimu ilivyobadili mtazamo wao hasi dhidi ya watu wengine

Nafasi ya elimu katika kuchagiza amani miongoni mwa wakimbizi na  jamii zinazowahifadhi imedhihirika huko Uganda wilayani Kikuube magharibi mwa nchi ambako kuna makazi ya wakimbizi ya Kyangwali. Hilo limethibitika wakati huu dunia kesho Januari 24 ikiadhimisha siku ya elimu duniani maudhui yakiwa kujifunza kwa ajili ya amani.