Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Palestina. Familia ikipika kwenye kifusi cha nyumba yao
© WFP/Ali Jadallah

Habari kwa ufupi: Gaza, Sudan, Uchaguzi Mkuu DR Congo

Mashirika ya Umoja wa Mataifa leo yameendelea kusisitiza wito wa usitishwaji mapigano katika ukanda wa Gaza kwani hali inazidi kuwa mbaya kila uchao, lile la afya duniani WHO limesema timu yake ilifanikiwa kufika katika hospitali za Al Ahil Arab na Al Shifa Gaza kaskasini na uharibifu walioushuhudia hauelezeki.

Familia ya Wapalestina waliokimbia makazi sasa wanaishi katika kambi ya muda kusini mwa Gaza bila maji, umeme, au chakula cha kutosha.
WFP/Ali Jadallah

Msaada wa kwanza kupitia Jordan wafikishwa Gaza

Baada ya wiki za mipango kwa pande zote, hatua hii ya kwanza muhimu ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) kuweza kuvusha misaada inaweza kufungua njia ya ukanda wa misaada endelevu zaidi kupitia Jordan na kuruhusu utoaji wa misaada zaidi. Hilo hadi sasa halijawezekana isipokuwa kwa njia moja tu kupitia Misri. 

Uchaguzi wa rais na wabunge unafanyika katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
MONUSCO/Michael Ali

Uchaguzi mkuu DRC wafanyika kama ilivopangwa

Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, uchaguzi mkuu wa Rais, Magavana, wabunge na madiwani umefanyika hii leo kama ilivyopangwa licha ya changamoto zilizojitokeza katika maeneo mbalimbali ya nchi hiyo. Assumpta Massoi amefuatiliana na kutuandalia ripoti hii. 

Sauti
1'47"
Kampeni ya chanjo ya Polio nchini Tanzania.
UNICEF TANZANIA

Chanjo ya polio sio tu inamlinda mtoto bali inaokoa maisha: UNICEF

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF linahimiza kila nchi kuhakikisha watoto wote wenye umri wa chini ya miaka 5 wanapatiwa chanjo dhidi ya polio ugonjwa ambao sio tu unasababisha ulemavu kwa watoto lakini pia ukakatili maisha yao. Kwa msaada kutoka wakfu wa Bill na Melinda gates hivi karibuni UNICEF na shirika la afya duniani WHO nchini Tanzania walizindua kampeni kubwa ya chanjo dhidi ya ugonjwa huo iliyowafikia watoto zaidi ya milioni 4.

Sauti
2'17"
Watu waliotawanywa na mchafuko Sudan wakivuka mpaka kwenda Sudan Kusini
© UNHCR/Ala Kheir

Janga la watu kutawanywa Sudan linaongezeka huku machafuko yakisambaa: UNHCR

UNHCR, Shirika la Umoja wa Msataifa la Kuhudumia Wakimbizi UNHCR, limesema linasikitishwa na janga la watu kuendelea kuzamikika kuyahama makazi yao nchini Sudan na kukimbilia nchi jirani huku mamia ya maelfu ya watu wakikimbia mapigano ya hivi karibuni kabisa katika jimbo la Al Jazirah katikati mwa Sundan jimbo lililo, kusini mashariki mwa mji mkuu, Khartoum