Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Zaidi ya watu 12,000 wameripotiwa kukimbia Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR na kuingia nchini DR Congo.
© UNHCR/Ghislaine Nentobo

UNHCR yatiwa hofu na wanaokimbia ghasia CAR

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR limesema lina hofu kubwa ya kwamba ghasia na ukosefu wa usalama vitokanavyo na uchaguzi mkuu wa tarehe 27 mwezi uliopita nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR, vimesababisha zaidi ya watu 30,000 kukimbilia nchi jirani za Cameroon, Chad, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na Jamhuri ya Congo.

 

Manusura wa mauaji ya kimbari ya Rwanda Liberée Kayumba, mwenye umri wa miaka 24, na mfanyakazi wa WFP anayesaidia wakimbizi wanaokimbilia nchi yake.
WFP/Jonathan Eng

Lishe ya WFP iliniokoa, sasa natumikia WFP kusaidia wengine- Liberee Kayumba

Wahenga walinena ukishikwa shikamana, na ndivyo anavyofanya Liberee Kayumba ambaye ni manusura wa mauaji ya kimbari ya Rwanda dhidi ya Watutsi yaliyofanyika mwaka 1994, anasema yuko hai leo hii sababu ya msaada wa chakula wa shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula WFP , ambao ulimuhamasisha baadaye kujiunga na shirika hilo kusaidia wakimbizi wa Burundi kama alivyosaidiwa.

Sauti
2'12"