UNHCR yatiwa hofu na wanaokimbia ghasia CAR
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR limesema lina hofu kubwa ya kwamba ghasia na ukosefu wa usalama vitokanavyo na uchaguzi mkuu wa tarehe 27 mwezi uliopita nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR, vimesababisha zaidi ya watu 30,000 kukimbilia nchi jirani za Cameroon, Chad, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na Jamhuri ya Congo.