Haiti: Ukosefu wa fedha unaweka rehani maisha ya watoto 86,000
Idadi ya Watoto chini ya miaka 5 wanaougua utapiamlo mkali nchini Haiti inaweza kuongezeka zaidi ya mara mbili mwaka huu, ameonya Jean Gough mkurugenzi wa shirika la Umoja wa Mataifa la Watoto – UNICEF katika ukanda wa Amerika kusini na karibiani, wakati akihitimisha ziara yake ya siku 7 katika nchi hiyo.