Katibu Mkuu wa UN alaani vikali ukandamizaji nchini Myanmar.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres, analaani vikali ukandamizaji nchini Mynmar, imeeleza taarifa iliyotolewa hii leo Jumapili kupitia msemaji wake mjini New York, Marekani.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres, analaani vikali ukandamizaji nchini Mynmar, imeeleza taarifa iliyotolewa hii leo Jumapili kupitia msemaji wake mjini New York, Marekani.
Shirika la kuhudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa, UNHCR, kupitia taarifa yake iliyotolewa hii leo mjini Geneva Uswisi, limesema linasikitishwa sana na msururu wa ujumbe wa kusikitisha ambao limekuwa likipokea kutoka kwa kikundi cha waomba hifadhi 10 ambao hivi sasa wamewekwa kizuizini katika eneo la Mutukula, kaskazini magharibi mwa Tanzania.
Mwakilishi wa shirika la kuhudumia watoto la Umoja wa Mataifa UNICEF Nigeria, Peter Hawkins kupitia taarifa iliyotolewa hii leo katika mji mkuu wa Nigeria, Abuja, amesema amefarijika kupokea habari iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu ya kuachiliwa kwa wanafunzi 27 wa Chuo cha Sayansi cha Serikali huko Kagara, ambao walitekwa nyara kutoka shule yao zaidi ya wiki moja iliyopita na kwamba anatarajia kurudi kwao salama katika familia zao.
Mkurugenzi Mkuu wa shirika la afya la Umoja wa Mataifa amesema amefarijika na hatua ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa leo kupiga kura na kupitisha azimio la kutaka pande zote katika mizozo kusitisha uhasama ili kutoa fursa ya kutoa chanjo dhidi ya corona au Covid-19 na misaada mingine ya kibinadamu.
Côte d'Ivoire imekuwa nchi ya pili baada ya Ghana, kupokea dozi za chanjo dhidi ya ugonjwa wa Corona au COVID-19 kupitia mfumo wa kimataifa wa COVAX wa kusaka na kusambaza chanjo hizo kwa nchi za kipato cha chini na kati.
Mataifa hayajafikia popote katika kiwango kinachotakiwa kukabili ongezeko la joto duniani, imesema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa iliyotolewa hii leo huku ikisihi serikali kuchukua hatua thabiti zaidi na za kina ili kufikia malengo ya mkataba wa Paris wa mabadiliko ya tabianchi ya kuhakikisha ongezeko la joto halizidi nyuzijoto 1.5 katika kipimo cha Selsiyasi ifikapo mwishoni mwa karne hii.
Hii leo katika jimbo la Zamfara kaskazini-magharibi mwa Nigeria, zaidi ya watoto 300 hawajulikani waliko baada ya watu wenye silaha kushambulio shule yao, tukio ambalo limelaaniwa vikali na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF.
Mkurugenzi Mtendaji wa Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kukabili uhalifu na madawa ya kulevya, UNODC, Ghada Waly amezindua dira ya mkakati wa Afrika kwa mwaka 2030, uzinduzi uliofanyika kimtandao hii leo wakati wa mkutano wa ngazi ya juu.
Kikundi cha walinda amani wanawake kutoka Tanzania katika kikosi cha nane kinachohudumu katika Ujumbe wa Umoja wa Mataifa FIB MONUSCO, nchini DRC, kimewatembelea wanawake wa kata za Matembo, Nzuma na Ngadi wilaya ya Beni.
Umoja wa Mataifa na jumuiya ya kiuchumi ya nchi za Afrika Magharibi ECOWAS leo wamelaani machafuko nchini Niger kufuatia tangazo la matokeo ya awali ya duru ya pili ya uchaguzi wa rais tarehe 21 Februari.