Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Tanzania
World Bank/Hendri Lombard

Tanzania yawaweka kizuizini wasaka hifadhi, UNHCR yatafuta njia ya kufikia suluhu.  

Shirika la kuhudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa, UNHCR, kupitia taarifa yake iliyotolewa hii leo mjini Geneva Uswisi, limesema linasikitishwa sana na msururu wa ujumbe wa kusikitisha ambao limekuwa likipokea kutoka kwa kikundi cha waomba hifadhi 10 ambao hivi sasa wamewekwa kizuizini katika eneo la Mutukula, kaskazini magharibi mwa Tanzania.  

Wanafunzi akiwa darasani Nigeria.
© UNICEF/Apochi Owoicho

UNICEF yafarijika kupokea habari za kuachiliwa wanafunzi 27 waliotekwa Kagara, Nigeria.  

Mwakilishi wa shirika la kuhudumia watoto la Umoja wa Mataifa UNICEF Nigeria, Peter Hawkins kupitia taarifa iliyotolewa hii leo katika mji mkuu wa Nigeria, Abuja, amesema amefarijika kupokea habari iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu ya kuachiliwa kwa wanafunzi 27 wa Chuo cha Sayansi cha Serikali huko Kagara, ambao walitekwa nyara kutoka shule yao zaidi ya wiki moja iliyopita na kwamba anatarajia kurudi kwao salama katika familia zao. 

Watu wanaoishi katika visiwa vya Comoro kwenye bahari ya Indi wanahitajhi kuhimili mabadiliko ya tabianchi.
UNDP Comoros/James Stapley

Ripoti ya tabianchi ni onyo kwa sayari- Guterres

Mataifa hayajafikia popote katika kiwango kinachotakiwa kukabili ongezeko la joto duniani, imesema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa iliyotolewa hii leo huku ikisihi serikali kuchukua hatua thabiti zaidi na za kina ili kufikia malengo ya mkataba wa Paris wa mabadiliko ya tabianchi ya kuhakikisha ongezeko la joto halizidi nyuzijoto 1.5 katika kipimo cha Selsiyasi ifikapo mwishoni mwa karne hii.