Kuna matumaini ya kasi mpya katika kupambana na ukoma, lakini unyanyapaa unaendelea.
Ikiwa leo ni siku ya ukoma ulimwenguni, wataalam wanataka kukomeshwa kwa ubaguzi na unyanyapaa unaoendelea dhidi ya watu wenye ugonjwa huo.
Ikiwa leo ni siku ya ukoma ulimwenguni, wataalam wanataka kukomeshwa kwa ubaguzi na unyanyapaa unaoendelea dhidi ya watu wenye ugonjwa huo.
Ofisi ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa OHCHR leo imeitaka serikali ya Iran kusitisha mara moja hatua ya kutaka kumnyonga raia wa nchi hiyo anayedaiwa kuteswa hadi kukiri kwamba ni mwanachama wa kundi la jihadi.
Mwaka mmoja tangu ugonjwa wa Corona au COVID-19 utangazwe kuwa dharura ya afya ya umma duniani, bado gonjwa hilo limesalia kuwa hatari na kutishia siyo tu nchi maskini bali pia tajiri.
Shirika la mpango wa chakula la Umoja wa Mataifa, WFP linaimarisha msaada kwa watu waliofurushwa makwao baada ya mapigano ya kikabila magharibi na kusini mwa Darfur nchini Sudan kusababisha watu 100,000 kukimbia ili kusaka usalama.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema chanjo dhidi ya corona au COVID-19 ni muhimu ili kuhakikisha kila mtu kila mahali yuko salama dhidi ya janga hili hatari.
Mwaka 2020 ulikuwa ni mwaka wa majanga lakini 2021 ni mwaka wa fursa na matumaini! Ni kauli ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres aliyotoa leo kwa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani akielezea vipaumbele vyake 10 kwa mwaka 2021.
Wazazi nchini Tanzania wameupokea vizuri mradi unaotekelezwa na mashirika matatu ya Umoja wa Mataifa, lile la elimu, sayansi na utamaduni, UNESCO, la masuala ya idadi ya UNFPA na la wanawake UN Women, ambao unalenga kuwawezesha wasichana kupitia elimu. Baada ya jana kuwaangazia wasichana wanufaika wa mradi huu, leo, Ahimidiwe Olotu ametuandalia sehemu ya pili inayoangazia wazazi na wanajamii kwa ujumla.
Wakati zahma zikiongezeka Afrika Kusini mwa jangwa la Sahara na kuwalazimisha mamilioni ya watu kufungasha virago, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR limetoa raia ya kuongeza juhudi za kuwasaidia wakimbizi na wahamiaji hasa wanaobidi kupitia njia hatari kwenye bahari ya Mediterrania kwenda kusaka mustakbali bora.
Hatimaye matokeo ya kura ya maoni iliyoendeshwa na Umoja wa Mataifa kwa wakazi wa dunia kuhusu udharura wa janga la tabianchi yametolewa hii leo huku asilimia 64 ya washiriki wakitambua umuhimu wa hatua za dharura dhidi ya mabadiliko ya tabianchi na hivyo kuwepo kwa hatua mahsusi za makusudi ili kukabili janga la tabianchi linalokumba dunia hivi sasa.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema katika kuwakumbuka waathirika milioni sita ambao ni Wayahudi na wengineo waliouawa kikatili wakati wa mauaji ya maangamizi makuu ya Holocust chini ya utawala wa Kinazi na washirika wao, inasikitrisha kwamba chuki dhidi ya Wayahudi bado inaendelea.