COP26 ikifungua pazia WMO yasema miaka 7 iliyopita imevunja rekodi ya joto duniani
Miaka saba iliyopita inaelekea kuwa ya joto zaidi kuwahi kurekodiwa sanjari na kupanda kwa kina cha bahari ni katika viwango vya kuvunja rekodi, kulingana na ripoti ya muda ya shirika la hali ya hewa duniani (WMO) ya hali ya hewa duniani kwa mwaka 2021, iliyotolewa Jleo umapili, wakati mkutano wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabianchi COP26, ukifunguliwa Glasgow, Uingereza.