Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Mabadiliko ya tabianchi yameongeza hatari ya hali ya hewa kavu, ya joto ambao inachangia kuchochea moto wa nyika
Unsplash/Mikhail Serdyukov

COP26 ikifungua pazia WMO yasema miaka 7 iliyopita imevunja rekodi ya joto duniani

Miaka saba iliyopita inaelekea kuwa ya joto zaidi kuwahi kurekodiwa sanjari na kupanda kwa kina cha bahari ni katika viwango vya kuvunja rekodi, kulingana na ripoti ya muda ya shirika la hali ya hewa duniani (WMO) ya hali ya hewa duniani kwa mwaka 2021, iliyotolewa Jleo umapili, wakati mkutano wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabianchi COP26, ukifunguliwa Glasgow, Uingereza.

Cap Haitien mji ulio pani ya Kaskazini ya Haiti kabla ya machafuko ya sasa ya kisiasa
MINUJUSTH/Leonora Baumann

Tukiadhimisha siku ya miji tudhibiti hatari za mabadiliko ya tabianchi na kujenga mnepo:UN 

Leo ni siku ya miji duniani, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mastaifa amesema ingawa kupanda kwa kina cha bahari kunaweza kuweka zaidi ya watu milioni 800 katika miji ya pwani kwenye hatari ya moja kwa moja ifikapo mwaka 2050, chini ya asilimia 10 ya fedha za mabadiliko ya tabianchi kwa maeneo ya mijini zinakwenda katika hatua za kukabiliana na kujenga mnepo. 

Senegal ni moja kati ya nchi 6 zilizoathirika na ukame mkali mwaka huu
UNOCHA/Eve Sabbagh

Ukweli ulio wazi ni kwamba dunia inaelekea kwenye zahma ya mabadiliko ya tabianchi:Guterres

Tuko katika wakati muhimu kwa sayari yetu. Lakini wacha tuwe wazi  kuna hatari kubwa ambayo mkutano wa mabadiliko ya tabianchi wa Glasgow unaweza usizai matunda, ameonya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres hii leo akizungumza na waandishi wa Habari mjini Roma Italia kunakofanyika mkutano wa mataifa 20 yaliyoendelea kiuchumi duniani au G-20.

Mwanamke na watoto wake wakiume wakiwa wamesimama nje ya nyumba yao kwenye makazi ya wakimbizi wa ndani huko Baboua, Jamhuri ya Afrika ya Kati -CAR
© UNICEF/Florent Vergnes

Mshikamano wa kimataifa wahitajika kufikia amani na usalama Afrika:UN

Naibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa leo amesisitiza umuhimu wa amani na usalama barani Afrika, wakati akiwashukuru mabalozi katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwa kusaidia Umoja wa Mataifa kuangazia suala hilo, na jinsi nchi zote wanachama zinavyoweza kufanya kazi na Muungano wa Afrika AU, kanda zingine na vikundi vya kanda, ili kufanya maisha kuwa salama zaidi katika bara zima.