Nimejifunza kwamba kukirimu wakimbizi sio lazima uwe tajiri:Guterres
Tatizo la wakimbizi ni jukumu la kila mtu sio wakimbizi au nchi zinazowahifadhi pekee, kwani nimejifunza ukarimu sio lazima uendane na utajiri. Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa hii leo katika kongamano la kimatifa kwa ajili ya wakimbizi linaloendelea mjini Geneva Uswis.