Ushirikiano wa kimataifa unasalia kuwa nguzo ya suluhu ya kimataifa-Muhammad
Akitoa taarifa ya kufunga mjadala Mkuu wa wazi wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mjini New York hii leo Rais wa Baraza Kuu Tijjani Muhammad-Bande amesema ushirikiano wa kimataifa unasalia kuwa nguzo muhimu inayokubalika na kutegemewa katika kutatua changamoto za kimataifa miongoni mwa nchi wanachama.