Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa wa Burundi Ezechiel Nibigira akihutubia mjadala mkuu wa mkutano wa 74 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA74.
UN Photo/Cia Pak

Burundi yataka iondolewe kwenye ajenda ya Baraza la Usalama

Mjadala mkuu wa mkutano wa 74 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA74 ukitamatishwa hii leo  jiijni New York, Marekani, Waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa wa Burundi Ezechiel Nibigira amehutubia jukwaa hilo akitaka ajenda ya Burundi kwenye Baraza la Usalama iondolewe kwa kuwa hali ya usalama nchini humo ni tulivu.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres, (kulia) akiwa na Waziri wa Mambo ya nje wa Burundi  Ezéchiel Nibigira  baada ya mazungumzo yao jijini New York, Marekani
Picha ya UN /Eskinder Debebe

Burundi twafanya uchaguzi mwakani, tuungeni mkono- Waziri Nibigira

Waziri wa mambo ya nje wa Burundi Ezechiel Nibigira ameiambia Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa kuwa anakusudia baadaye hii leo kuuleza mjadala mkuu wa mkutano wa 74 wa Baraza kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA74 pamoja na mambo mengine, kuhusu hatua za maendeleo ambazo Burundi imepiga na pia kuiomba jumuiya ya kimataifa kuiunga mkono nchi yake.

Sauti
2'12"
Visiwa vya Tuvalu viko katika hatari ya kuongezeka kwa kina cha maji ya bahari kutokana na mabadiliko ya tabia nchi.
UNDP Tuvalu/Aurélia Rusek

Nchi 38 zinazoendelea za visiwa vidogo, ni kati ya nchi zilizo hatarini zaidi

Nchi 38 zilizotambuliwa na Umoja wa Mataifa kama nchi zinazoendelea za visiwa vidogo, au SIDS, ni kati ya nchi zilizo hatarini zaidi ulimwenguni. Nchi hizi ambazo ziko kwenye eneo la Karibea, bahari ya Pasifiki, ya Atlantiki, ya Hindi na Bahari ya Uchina ya Kusini zinaathirika na hali inayozidi ya mabadiliko ya tabianchi ulimwenguni ambayo haitabiriki. Pamoja na changamoto za mazingira, SIDS inakabiliwa na seti ya kipekee ya masuala yanayohusiana na udogo na umbali.