Mwaka mmoja wa Ebola DRC ukitimu, mashirika ya UN yaazimia kuchukua hatua zaidi
Kesho Agosti 1 ni mwaka mmoja tangu kuripotiwa kwa mlipuko wa 10 wa ugonjwa wa Ebola huko jimboni Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC.
Kesho Agosti 1 ni mwaka mmoja tangu kuripotiwa kwa mlipuko wa 10 wa ugonjwa wa Ebola huko jimboni Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC.
Tatizo la ajira kwa vijana ni moja ya mtihani mkubwa unaoikabili dunia hivi sasa ambayo inahitaji suluhu ya pamoja kuitatua limesema shirika la kazi duniani ILO.
Mgonjwa wa pili wa Ebola aliyebainika na kuthibitishwa jana huko Goma jimboni Kivu, Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC amefariki dunia.
Taasisi za kiraia zimeendelea kushirikiana na serikali hususan katika nchi zinazoendelea ili kuweka mazingira bora ya kazi maeneo ya vijijini kwa wahudumu wa afya na hivyo kufanikisha lengo namba 3 la malengo ya maendeleo endelevu kuhusu afya bora na ustawi kwa wote.
Serikli ya Uchina leo imetia saini makubaliano ya kuchangia dola milioni moja kwa shirika la Umoja wa Mataifa la msaada wa wakimbizi wa Kipalestina UNRWA.
Kuzalisha chakula cha kutosha sio tatizo, tatizo ni fursa ya watu kupata chakula kilichopo ili kupambana na njaa na utapiamlo.
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR limesema manusura 116 wa ajali ya boti ya wiki iliyopita waliokuwa wakishikiliwa hadi leo Jumatano Julai 31 ndani ya boti ya ukozi ya Italia kwenye bandari ya Sicily wameruhusiwa kuteremka kutoka kwenye boti hiyo.
Ofisi ya Kamishna mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa, OHCHR, kupitia msemaji wake Rupert Colville imesema inasikitishwa sana na hali ya mtoto mpalestina Abdul Rahman Shteiwi ambaye alipigwa risasi kichwani na vikosi vya usalama vya Israel (ISF) mnamo tarehe 12 ya mwezi huu wa Julai katika kile kinachoonekana kuwa mfano wa matumizi makubwa ya nguvu.
Mwaka 2018 umeongoza kwa kuwa na idadi kubwa zaidi ya watoto waliouawa au waliokatwa viungo kwenye maeneo ya mizozo tangu Umoja wa Mataifa uanze kufuatilia na kuripoti uhalifu mkubwa kwenye vita, imesema ripoti iliyotolewa leo na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu watoto kwenye mizozo.
Ili kutatua changamoto kubwa zinazoikabili dunia hivi sasa kuanzia umaskini, mabadiliko ya tabianchi na hata majanga ya asili tunahitaji utashi, hatua zaidi na hatua zenyewe zichukuliwe sasa. Kauli hiyo imetolewa na bingwa kijana wa mwaka 2017 wa kupigania maslahi ya dunia Mariama Mamane kutoka Burkina Faso. Tupate maelezo zaidi na Jason Nyakundi