Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Mtoto wa umri wa miaka 12 akipita pembezoni mwa nyumba iliyobomolewa na mashambulizi kutoka angani yaliyofanywa na Israeli katika jiji la Rafah, kusini mwa Gaza mwaka 2012.
UNICEF/UNI132737/El Baba

Waliomjeruhi mtoto mpalestina Abdul Rahman Shteiwi wafikishwe mbele ya sheria- OHCHR

Ofisi ya Kamishna mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa, OHCHR, kupitia msemaji wake Rupert Colville imesema inasikitishwa sana na hali ya mtoto mpalestina Abdul Rahman Shteiwi  ambaye alipigwa risasi kichwani na vikosi vya usalama vya Israel (ISF) mnamo tarehe 12 ya mwezi huu wa Julai katika kile kinachoonekana kuwa mfano wa matumizi makubwa ya nguvu.