Katibu Mkuu Guterres na viongozi wengine waandamizi wa UN waonesha mshikamano na DR Congo katika ziara ya siku tatu
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres na viongozi wengine waandamizi wa Umoja wa Mataifa hii leo wameanza ziara ya siku tatu nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC ambako wananchi wanakabiliwa na ukosefu wa usalama na janga la afya linaloendelea ikiwemo Ebola ambayo imeshawaua watu 2000.