Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Balozi mwema mpya wa UNHCR Mercy Masika Muguro akiwa nje ya duka kwenye kambi ya wakimbizi ya Kakuma nchini Kenya
© UNHCR/Will Swanson

Miongoni mwa tulizokuwa nazo wiki hii

Mtoto mmoja mhamiaji hufariki dunia au kupotea kila siku, UN yataka ulinzi zaidi. Chonde chonde wasafiri pateni chanjo dhidi ya Surua imesisitiza WHO. Kuongeza ushindani wa SMEs ni muarobaini wa kufanikisha SDGs imeeleza Ripoti. Ripoti nyingine imesema familia nyingi za mzazi mmoja duniani zinaongozwa na wanawake. Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR, limeteua muimbaji nyota wa nyimbo za injili Mercy Masika kuwa balozi.

Wahamiaji wakirudi nyumbani kwa msaada wa IOM
IOM

Wahamiaji wana haki na wanasitahili usaidizi-Nick Ogutu

Mkutano wa 16 wa kuhusu haki za binadamu, uhamiaji na vijana leo umeingia siku yake ya pili katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani. Mkutano huo wa kimataifa unaofanyika kila mwaka unawakutanisha wadau wa haki za binadamu kutoka kote duniani na mmoja wa waliohudhuria ni rais wa taasisi inayoitwa ‘Safari yangu’, inayosimamiwa na Chuo Kikuu cha Columbia cha hapa Marekani, Bwana Nick Ogutu.

Sauti
1'39"