Mabunge thabiti ni msingi mkuu wa demokrasia na maendeleo
Leo ni siku ya mabunge duniani ambapo Umoja wa Mataifa unaeleza umuhimu wa mabunge hayo katika kupaza sauti za wananchi.
Leo ni siku ya mabunge duniani ambapo Umoja wa Mataifa unaeleza umuhimu wa mabunge hayo katika kupaza sauti za wananchi.
Dunia inakabiliwa na dharura ya tabianchi, amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres wakati akihutubia mkutaon huko Abu Dhabi nchini Saudi Arabia hii leo akisihi washiriki watumie fursa ya sasa kuchukua hatua dhidi ya tabianchi.
Umoja wa Mataifa pamoja na Ufaransa na China wamesisitiza ahadi yao thabiti ya kuendeleza ushirikiano wa kimataifa ili kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi ikiwemo utekelezaji wa mkataba wa mabadiliko ya tabianchi.
Mtoto mmoja mhamiaji hufariki dunia au kupotea kila siku, UN yataka ulinzi zaidi. Chonde chonde wasafiri pateni chanjo dhidi ya Surua imesisitiza WHO. Kuongeza ushindani wa SMEs ni muarobaini wa kufanikisha SDGs imeeleza Ripoti. Ripoti nyingine imesema familia nyingi za mzazi mmoja duniani zinaongozwa na wanawake. Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR, limeteua muimbaji nyota wa nyimbo za injili Mercy Masika kuwa balozi.
Takribani watoto 1,600 waliripotiwa kufariki dunia au kupotea kati yam waka 2014 hadi 2018, imesema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa iliyotolewa leo, ikimanisha kuwa kwa wastani, mtoto mmoja alitoweka kila siku.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema mkutano wa kundi la mataifa 20, G20 unafanyika wakati ambapo shaka na shuku zimekumba dunia nzima katika nyanja zote kuanzia kiuchumi, kisiasa na kijamii.
Takribani watu 117 waliuawa kwenye jimbo la Ituri nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRc kati ya tarehe 10 na 13 mwezi huu wa Juni kutokana na mapigano kati ya kabila la wahema na walendu.
Shirika la afya ulimwenguni WHO limewapongeza wahudumu wa afya na wizara ya afya ya Uganda kwa hatua za haraka na maandalizi ya kupambana na mlipuko wa Ebola uliozuka hivi karibuni nchini humo.
Mkutano wa 16 wa kuhusu haki za binadamu, uhamiaji na vijana leo umeingia siku yake ya pili katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani. Mkutano huo wa kimataifa unaofanyika kila mwaka unawakutanisha wadau wa haki za binadamu kutoka kote duniani na mmoja wa waliohudhuria ni rais wa taasisi inayoitwa ‘Safari yangu’, inayosimamiwa na Chuo Kikuu cha Columbia cha hapa Marekani, Bwana Nick Ogutu.
Viongozi 11 wa mashirika ya misaada ya kibinadamu ya Umoja wa Mataifa na wadau wao wamezindua kampeni ya kimataifa ya kuonesha mshikamano na wananchi wa kaskazini-magharibi mwa Syria ambao hivi sasa wanakabiliwa na mashambulizi makubwa ya kijeshi.