Mashambulizi huko Beni ni ya kupanga hivyo lazima watekelezaji wawajibishwe- Lacroix
Akiwa ziarani jimboni Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, mkuu wa operesheni za ulinzi wa amani kwenye Umoja wa Mataifa, Jean-Pierre Lacroix amesema mashambulizi dhidi ya walinda amani na wafanyakazi wa kibinadmu nchini humo si vitu vya ghafla bali ni matukio ya kupangwa na yanafadhaliwa na hivyo hayapaswi kukwepa mkono wa sheria.