Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Wafanyakazi wa WHO kitengo cha kupambana na Ebola wakifika eneo la Komanda, Jimbo la Ituri mashariki mwa DRC, Januari 2019.
WHO/Lindsay Mackenzie

Kuna ongezeko la maambukizi ya Ebola DRC-WHO.

Shirika la Afya duniani WHO limetoa ripoti katika tovuti yake ikisema wiki hii kumeshuhudiwa ongezeko la maambukizi ya mlipuko wa Ebola unaoendelea nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC katika eneo la Kivu Kaskazini na Ituri. Katika kipindi hiki vikundi vya wataalamu wa kudhibiti Ebola vinakabiliana na changamoto za kila siku katika kuhakikisha utambuzi kwa wakati na ufuatiliaji wa maambukizi yote katikati mwa vurugu za makundi yenye silaha na pia kutoaminiana miongoni mwa jamii zilizoathirika.