Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Baba akiwa na mwanae kwenye kambi ya wakimbizi kutoka Syria nchini Jordan.
UNHCR/A. Eurdolian

Msimu wa baridi, madhila zaidi ya wakimbizi wa Syria nchini Jordan

Miezi ya msimu wa baridi kali ikinyemelea, ni kumbukizi nyingine ya madhila kwa wakimbizi wa Syria waliosaka hifadhi Jordan ambao wengi wao wanaishi katika mazingira magumu wakati huu ambapo inaelezwa kuwa juhudi za shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR na wadau wake Jordan za kuwapatia vifaa vya kukabiliana na joto zinaonekana kuwa muhimu zaidi.  Taarifa zaidi na Siraj Kalyango.

Ismail Isack Amin, mkulima mwenye umri wa miaka 66 ambaye anasema amekuwa akijinufaisha na ardhi  yenye rutuba nchini mwake Somalia tangu akiwa na umri wa miaka
UNSOM video screen capture

Ardhi imesalia kuwa mkombozi wangu- Mkulima Somalia

Nchini Somalia, harakati za kuhakikisha wananchi wanashiriki kwenye shughuli za kiuchumi na kijamii zinaendelea kuzaa matunda kwa wananchi ambapo ofisi ya Umoja wa Mataifa nchini  humo, UNSOM inadhihirisha juhudi hizo kupitia mfululizo wa video zinazonesha wananchi wakishiriki harakati mbalimbali. 

Shirika la chakula duniani, WFP likisambaza mgao wa chakula katika jimbo la Ituri, DRC ambako maelfu ya watu wamekimbia machafuko ya kikabila mnamo 21 Machi 2018.
WFP/Jacques David

Idadi ya waliofikishiwa msaada na WFP nchini DRC mwaka 2018 imeongezeka maradufu

Kadri machafuko yalivyozidi kuenea mwaka 2018, pamoja na idadi kubwa ya watu waliopoteza makazi na kiwango kidogo cha  mavuno kilichoambatana na umaskini, hali iliyosababisha idadi ya watu wanaokabiliwa na uhaba wa chakula nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo,  DRC kufikia milioni 13.1, shirika la mpango wa chakula duniani WFP lililazimika kuongeza operesheni zake nchini  humo na kufikia watu milioni 5.

Mwendesha mashtaka mkuu wa Mahakama ya  ICC
UN Photo/Rick Bajornas)

DRC Jiepusheni na uhalifu wakati wa uchaguzi la sivyo mtawajibishwa- ICC

Kuelekea uchaguzi mkuu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC tarehe 23 mwezi huu, mahakama ya kimataifa ya uhalifu, ICC imeonya kuwa yeyote yule nchini humo ambaye atachochea, ama atashiriki katika fujo kwa kuamuru, kutaka ama kuhimiza au kuchangia kwa njia yoyote ile au kutenda makosa yaliyo chini ya mamlaka ya ICC atashtakiwa na kufikishwa mbele ya mahakama. 

Daktari mkimbizi kutoka Syria amtibu mgonjwa akiwa ukimbizini.
© UNHCR/Claire Thomas

Mkataba wa Uhamiaji ukitekelezwa vizuri utalinda haki za wahamiaji.

Taarifa ya wataalamu wa Umoja wa Mataifa iliyotolewa hii leo mjini Geneva Uswisi imesema watalaam hao wameupokea wito uliotolewa katika mkataba wa kimataifa wa uhamiaji salama, wenye mpangilio na unaofuata kanuni za kawaida ambao umepitishwa mjini Marrakesh,Morocco hivi karibuni.

Wito huo umezitaka nchi kushirikiana na sekta binafsi katika kulinda haki za wahamiaji na kuhakikisha wanagawana faida za kiuchumi wanazozalisha.