Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Dawa za kupunguza makali ya UKIMWI-ARV
Photo: Sean Kimmons/IRIN

Upimaji VVUkwa wakati ni muhimili wa afya ya wafanyakazi- ILO

Katika takribani nchi 50 duniani imebainika kwamba maambukizi ya Virusi Vya Ukimwi au VVU yanaongezeka na idadi ya vifo vitokanavyo na ugonjwa huo bado iko juu. Hayo ni kwa mujibu wa ripoti ya karibuni ya shirika la kazi duniani ILO iliyotolewa kuelekea siku ya ukimwi duniani itakayoadhimishwa kote duniani  tarehe Mosi disemba.

Kutoka katika mtumbwi, kijana akitizama mto karibu na Sirajganj Bangladesh,eneo ambalo limeathirika na mmomonyoko uliowaacha wengi bila makazi.
IOM/Amanda Nero

Fahamu wa kina mkutano wa kimataifa wa mabadiliko ya tabianchi COP24

Wakati kiwango cha joto kikiendelea kupanda duniani , hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi zinazorota na fursa ya kulishinda jinamizi hili inaendelea kuwa finyu. Jumapili wiki hii Umoja wa Mataifa utaanza majadiliano muhimu ya jinsi gani ya kushughulikia tatizo hilo kwa pamoja na kwa haraka, katika wiki mbili za mkutano wa 24 wa mkataba wa kimataifa wa mabadiliko ya tabianchi, COP 24 utakaofanyika mjini Katowice nchini Poland.