Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

UN News/Siraj Kalyango

Msikate miti hovyo kwa kuwa jangwa lanyemelea

Ukataji holela wa miti kinyume na vibali ambavyo vinatolewa na serikali ni moja ya sababu za uharibifu wa mazingira nchini Kenya, amesema Isabella Masinde mtaalam wa mazingira, kutoka idara ya mazingira nchini humo.

Katika mahojiano  na Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa  Mataifa mjini New York, Marekani, Bi.Masinde,Mkurugenzi wa Mazingira na ulinzi wa masuala ya  kijamii katika kamati ya kitaifa ya kupokea  malalamiko kuhusu mazingira nchini Kenya amesema.miongoni mwa mengine kuwa maendeleo yanaathiri mazingira   wakati ..mambo ya kufanya mipango ya matumizi ya hayo mazingira hayatekelezwi, lakini kama kungekuwa na utaratibu wa kujua kama kwa mfano miti ikitolewa miti elfu moja tutaendelea vizuri.

Watoto wakiwa wamevalia tisheti zenye ujumbe wa kuungana dhidi ya chuki, wakati wa kuwakumbuka waliouawa katika sinagogi.
UN Photo/Rick Bajornas)

Guterres aongoza kumbukizi ya waliouawa Pittsburg

Jijini New York Marekani hii leo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ameungana na viongozi wengine wa dini na wakazi wa jiji hilo kukumbuka watu 11 waliopoteza maisha katika shambulio la mwishoni mwa wiki kwenye sinagogi moja huko Pittsburg, jimboni Pennyslvania nchini Marekani.