Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres
Picha ya UN /Rick Bajornas

Mauaji ya Gaza leo lazima yachunguzwe: Guterres

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ametoa wito wa kufanyika uchunguzi huru na wa wazi dhidi ya machafuko yaliyozuka leo Ijumaa kwenye uzio wa Gaza kati ya Wapalestina waliokuwa wakishiriki maandamano na vikosi vya ulinzi vya Israel na kusababisha vifo vya watu 15 na wengine wengi kujeruhiwa.

Wajumbe wakiwa katika ukumbi wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
UN/Eskinder Debebe

Damu iliyomwagika leo Gaza inatosha

Naibu msaidizi wa Katibu Mkuu kuhusu masuala ya kisiasa Tay Brook Zerhoun ametoa wito kwa vikosi vya usalama vya Israel kujizuia ili kuepuka zahma zaidi kwa raia wa Gaza, akisisitiza kuwa matumizi ya nguvu iwe ni suluhu ya  mwisho, na kutaka uchunguzi wa kina ufanyike dhidi ya mauaji yaliyotokea.