Mauaji ya Gaza leo lazima yachunguzwe: Guterres
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ametoa wito wa kufanyika uchunguzi huru na wa wazi dhidi ya machafuko yaliyozuka leo Ijumaa kwenye uzio wa Gaza kati ya Wapalestina waliokuwa wakishiriki maandamano na vikosi vya ulinzi vya Israel na kusababisha vifo vya watu 15 na wengine wengi kujeruhiwa.