Mzozo wa Yemen ni ‘mwiba’ kwa mama na mtoto
Mzozo nchini Yemen ukiwa umedumu kwa miaka minne sasa, wananchi wanaelezea vile ambavyo mazingira yamekuwa magumu kiasi kwamba hawawezi kukidhi mahitaji muhimu ya kila siku ikiwemo chakula.
Mzozo nchini Yemen ukiwa umedumu kwa miaka minne sasa, wananchi wanaelezea vile ambavyo mazingira yamekuwa magumu kiasi kwamba hawawezi kukidhi mahitaji muhimu ya kila siku ikiwemo chakula.
Harakati za ujenzi wa Somalia zikiendelea, wananchi wakiwemo wanawake wanachangia katika ukuaji wa uchumi wa nchi hiyo kwa kufanya biashara na kulipa kodi badala ya kusubiri misaada.
Shirika la kuhudumia wakimbizi duniani UNHCR linasema mji wa Vienna nchini Austria umeandaa nyumba, huduma za afya, madarasa ya lugha na programu za elimu kwa ajili ya wakimbizi na hivyo kuunga kampeni za shirika hilo za miji na manispaa zinazosaidia wakimbizi.
Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa maendeleo UNDP linafanya kazi kwa kushirikiana na serikali ya Peru na wananchi wanaofuatilia mazingira ili kutafuta mbinu za kuyarekebisha maeneo ambayo yamaethiriwa na uchimbaji wa mafuta katika msitu wa Amazon
Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Afghanistan UNAMA umelaani shambulio ambalo limetokea usiku wa kuamkia leo katika eneo la mji mkuu Kabul na kusababisha vifo na majeruhi.
Mtaalam Maalum wa Umoja wa Mataifa ameelezea wasiwasi wake mkubwa kufuatia tukio la mtoto wa kike mhamiaji kutoka Guatemala kufariki dunia mikononi mwa maafisa wa uhamiaji wa Marekani.
Idadi ya watu waliofariki dunia kutokana na tsunami iliyokumba maeneo ya mwambao mwa kisiwa cha Sumatra nchini Indonesia sasa imefikia 281 na wengine zaidi ya 1,000 wamejeruhiwa.
Nchini Ujerumani, mmiliki mmoja wa duka la kuoka mikate ameleta matumaini kwa vijana wakimbizi ambao awali walihisi maisha yao yametumbukia nyongo kutokana na changamoto walizokuwa wanakumbana nazo ikiwemo lugha na fursa za kujiendeleza. Grace Kaneiya na ripoti kamili.
Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa, UNEP linasema mkaa unaotengenezwa kwa kutumia kinyesi cha binadamu unadumu mara mbili zaidi ya mkaa wa kawaida na zaidi ya yote kiwango chake cha uchafuzi wa mazingira ni kidogo mno ikilinganishwa na kiwango cha uchafuzi wa hewa cha mkaa unaotokana na miti.
Mwaka 2018 ulighubikwa na changamoto nyingi hususan kwa nchi za Afrika, mizozo ikiendelea kukumba bara hilo sambamba na magonjwa. Hata hivyo kulikuwa na habari chanya, na kwa muhtasari tutaangazia pande zote za sarafu wakati huu ambapo tunafunga mwaka huu wa 2018.