Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Uchaguzi wa huru na haki utakuwa na maana kubwa kwa mstakabali wa watu wa Bangladesh kama kijana huyu ambaye pia ni dereva wa Lori
World Bank/Scott Wallace

Bangladesh hakikisheni mnafanya uchaguzi huru na wa haki: UN

Kuelekea uchaguzi mkuu nchini Bangladesh unaotarajiwa kufanyika jumapili hii ya tarehe 30 mwezi huu wa Desemba, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres kupitia taarifa iliyotolewa hii leo mjini New York Marekani na msemaji wake, amewasihi wadau wote Bangladesh wahakikishe wanaweka mazingira yasiyo na vurugu, vitisho wala kulazimishwa, kabla, wakati na baada ya uchaguzi, ili kuwezesha uchaguzi wa amani, halali na unaohusisha watu wote.