Wataalamu wa UN waitaka Sudan kuacha kutumia nguvu kubwa kuzuia maandamano ya amani.
Hii leo mjini Geneva, Uswisi, wataalamu wa Umoja wa Mataifa wameeleza hofu yao kuhusu kuongezeka kwa vurugu na kuuawa kwa waandamanaji nchini Sudan ambao wamekuwa wakipinga ongezeko la bei ya bidhaa na uhaba wa mafuta na chakula. Arnold Kayanda na maelezo zaidi.