Vita inayoendelea Gaza kwa miezi sasa ni usaliti dhidi ya ubinadamu: Griffiths
Mratibu mkuu wa misaada na masuala ya dharura wa Umoja wa Mataifa Martin Griffiths amesema vita inayoendelea Gaza imefikia harua ya kutisha.
Mratibu mkuu wa misaada na masuala ya dharura wa Umoja wa Mataifa Martin Griffiths amesema vita inayoendelea Gaza imefikia harua ya kutisha.
Maafisa wa Umoja wa Mataifa wameanza ziara ya tathmini huko Gaza na mashirika yao yataanza tena usambazaji wa misaada baadaye Alhamisi usiku baada ya sitisho la saa 48 kufuatia kitendo cha Israel kuua watumishi 7 wa kiutu kutoka shirika la World Central Kitchen kwenye eneo lililozingirwa la Gaza.
Chombo cha juu kabisa cha haki za binadamu cha Umoja wa Mataifa leo kimepitisha azimio kulaani madai ya "matumizi ya njaa kwa raia kama mbinu ya vita huko Gaza, huku pia kikitoa wito kwa Israel kuwekewa vikwazo vya silaha.”
Kesho kutwa jumapili ikiwa ndio itatimu miezi sita ya mzozo wa Gaza, huko Mashariki ya Kati, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres hii leo amezungumza na waandishi wa habari jijini New York, Marekani akirejelea wito wake wa sitisho la mapigano kwa misinigi ya kiutu, kuachiliwa kwa mateka wote bila masharti, ulinzi wa raia na misaada ya kiutu ifikie walengwa bila vikwazo vyovyote huku akikgusia pia Israeli kutumia akili mnemba kwenye operesheni zake.
Katika kuelekea miezi sita tangu kuanza mapigano mapya Ukanda wa Gaza Umoja wa Mataifa unasema zaidi ya mashambulizi 700 ya Israel dhidi ya Wapalestina yamerekodiwa katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa, ikiwa ni pamoja na Jerusalem Mashariki, katika kipindi cha takriban miezi sita iliyopita.
Mashirika ya kibinadamu ya Umoja wa Mataifa leo kwa mara nyingine yameonya kwamba bila dalili zozote za usitishaji mapigano Gaza hali ya kibinadamu inaendelea kuwa janga huku mashambulizi ya Israel yakiendelea kukatili maisha, kufurusha watu na kusababisha uharibifu usioelezeka na njaa nayo ikiongeza hofu ya hatma ya watu wa eneo hilo.
Leo maafisa wa masuala ya kibinadamu wa Umoja wa Mataifa wamelaani vikali mauaji ya wafanyakazi wa misaada 7 wa shirika lisilo la kiselikali au NGO la World Central Kitchen yaliyofanywa na jeshi la Israel, maafisa hao wakirejea kueleza hofu yao kwamba hakuna mahali palipo salia kuwa salama Gaza. Akizungumzia mauaji hayo Jamie McGoldrick, Mratibu wa masuala ya kibinadamu katika eneo linalokaliwa la Palestina amesema “Hili sio tukio la kipekee kwani hadi kufikia Machi 20 wahudumu wa kibinadamu 196 wameuawa Gaza tangu Oktoba 7 mwaka jana na hii ikiwa ni karibu mara tatu zaidi ya idadi ya vifo iliyorekodiwa katika mgogoro mmoja kwa mwaka."
Mratibu Mkuu wa Misaada ya kibinadamu na masuala ya dharura wa Umoja wa Mataifa Martin Griffiths amesema shirika la Umoja wa Mataifa la msaada kwa wakimbizi wa Kipalestina UNRWA ni uti wa mgongo wa operesheni za Kibinadamu Gaza hivyo jaribio la kulitenga shirika hilo lazima likome.
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi wa kipalestina (UNRWA) leo Machi 28 limetahadharisha kuhusu ujio wa baa la njaa katika Ukanda wa Gaza.
Hii leo Muhtasari wa Habari unamulika Gaza, Haiti na Sudan Kusini ambako kote ni majanga juu yamajanga na mwasilishaji wako ni Anold Kayanda