Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Mashariki ya Kati

Mvulana anakimbia katika mitaa iliyoharibiwa ya Gaza.
© UNRWA/Ashraf Amra

GAZA: Miezi 6 ya mzozo Guterres akemea matumizi ya Akili Mnemba

Kesho kutwa jumapili ikiwa ndio itatimu miezi sita ya mzozo wa Gaza, huko Mashariki ya Kati, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres hii leo amezungumza na waandishi wa habari jijini New York, Marekani akirejelea wito wake wa sitisho la mapigano kwa misinigi ya kiutu, kuachiliwa kwa mateka wote bila masharti, ulinzi wa raia na misaada ya kiutu ifikie walengwa bila vikwazo vyovyote huku akikgusia pia Israeli kutumia akili mnemba kwenye operesheni zake. 

Audio Duration
2'40"
Msaada wa chakula unaotolewa na World Central Kitchen ukipangwa kwenye boti inayoondoka Italia. (Maktaba)
© Open Arms

Gaza: UN yalaani vikali mauaji ya wahudumu 7 wa misaada ya kibinadamu

Leo maafisa wa masuala ya kibinadamu wa Umoja wa Mataifa wamelaani vikali mauaji ya wafanyakazi wa misaada 7 wa shirika lisilo la kiselikali au NGO la World Central Kitchen yaliyofanywa na jeshi la Israel, maafisa hao wakirejea kueleza hofu yao kwamba hakuna mahali palipo salia kuwa salama Gaza. Akizungumzia mauaji hayo Jamie McGoldrick, Mratibu wa masuala ya kibinadamu katika eneo linalokaliwa la Palestina amesema “Hili sio tukio la kipekee kwani hadi kufikia Machi 20 wahudumu wa kibinadamu 196 wameuawa Gaza tangu Oktoba 7 mwaka jana na hii ikiwa ni karibu mara tatu zaidi ya idadi ya vifo iliyorekodiwa katika mgogoro mmoja kwa mwaka."