Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Mashariki ya Kati

Mfanyakazi wa WFP akipakua misaada ya chakula ambacho kiko tayari kuliwa kutoka kwenye lori kribu na Alexandria Misri tayari kukiingiza Gaza chakula hicho
© WFP/Amira Moussa

Gaza: Maelfu wanavamia maghala ya Umoja wa Mataifa; ishara ya kukata tamaa baada ya mashambulizi ya wiki kadhaa

Mashirika ya misaada yameonya hii leo kwamba utaratibu wa kiraia unaanza kuvunjika huko Gaza baada ya maelfu ya watu waliokata tamaa kuvamia maghala yanayosimamiwa na Umoja wa Mataifa na vituo vingine vya usambazaji wa misaada katika eneo lililoharibiwa, wakichukua unga wa ngano, vifaa vya usafi na bidhaa nyingine muhimu za kujiokoa.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres akihutubia wanahabari mjini Kathmandu, Nepal.
UN Nepal

Hali huko Gaza 'inakuwa ya kukatisha tamaa kila saa', asema Mkuu wa Umoja wa Mataifa 

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ameanza ziara yake rasmi nchini Nepal kwa kutoa salamu za rambirambi kwa familia za wanafunzi 10 wa Nepal waliouawa katika mashambulizi ya kigaidi yaliyofanywa na Hamas nchini Israel, na kwa mara nyingine tena kutoa wito wa kulindwa kwa raia wote huko Gaza akisema, “hali inakua ya kukatisha tamaa kila saa.”