Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Eva Ghamaharo, mkazi wa Kaunti ya  Mto Tana, mnufaika wa mradi wa dharura wa mgao wa fedha kwa manusura wa mafuriko unaotekelezwa na UNICEF Kenya.
UNICEF/James Ekwam

Mafuriko Kenya: Mgao wa fedha waleta matumaini kwa wakazi wa Kaunti ya Mto Tana- UNICEF

Wingu kubwa la mvua likiwa limetanda kwenye mji wa Garsen, ulioko kaunti ya Mto Tana nchini Kenya, Eva Ghamaharo, mama wa watoto watatu anarejea nyumbani akitembea na watoto wake wawili mapacha wenye umri wa miaka mitatu baada ya kununua matumizi ya nyumbani kutoka kioski cha jirani. Watoto hawa wawili mapacha wa kike ni Grace na Jane na wanaonekana na furaha kwani angalau leo mama yao ameweza kuwanunulia kila mmoja pakiti ya maziwa na wanakunywa kwa furaha.

Sauti
2'6"
Watu waliokimbia makazi yao kutokana na migogoro wanaishi katika kambi ya muda karibu na Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
© WFP/Benjamin Anguandia

DRC: Mashambulizi Goma yaua raia 12, UN yalaani

Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, Bintou Keita amelaani vikali shambulio la leo la mabomu dhidi ya makazi mawili ya kuhifadhi wakimbizi wa ndani huko Lac-Vert na Mugunga takribani kilometa 13 hadi 15 kutoka Goma mji mkuu wa jimbo la Kivu Kaskazini.

Baadhi yao wamepumzika baada ya siku yenye shughuli nyingi kwenye Mkutano wa Viongozi wa Dunia.
UN News/Laura Quinones

Wanahabari wana jukumu muhimu la kuelimisha juu ya mabadiliko ya tabianchi: UN

Leo ni siku ya uhuru wa vyombo vya habari duniani mwaka huu ikibeba maudhui “Vyombo vya Habari kwa ajili ya Sayari: Uandishi wa habari katika kukabiliana na mgogoro wa mabadiliko ya tabianchi”  kwani Umoja wa Mataifa unasema mchango wa wanahabari na vyombo vya habari ni kiini katika kuhabarisha na kuelimisha umma kuhusu changamoto hiyo ya tabianchi. 

Sauti
2'23"
Mwanamke akipita kwenye maji ya mafuriko katika Jimbo la Hirshabelle, Somalia.
© WFP/Arete/Abdirahman Yussuf Mohamud

OCHA na wadau waanza kufikisha misaada kwa wakimbizi ili kujiandaa na mafuriko

Tukiwa katika msimu wa mvua kwa nchi nyingi za kusini mwa jangwa la Sahara, tuelekee nchini Somalia, Shirika la Umoja wa Mataifa la kuratibu misaada ya kibinadamu na masuala ya dharura, OCHA limesema wao na wadau wao wamejiandaa kufikisha mahitaji kwa watu 770,000 katika wilaya 22 za nchi hiyo ambao wanatarajiwa kuathirika na mvua za msimu huku wakieleza kuwa wakimbizi wa ndani wanatarajiwa kuaahirika ziadi. 

Sauti
2'17"