Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Vimbunga, mvua na mafuriko makubwa Afrika Mashariki UN itaendelea kusaidia

Naibu Rais Rigathi Gachagua (kushoto) akiandamana na ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa Kenya ukiongozwa na Mratibu Mkazi Dkt Stephen Jackson (kulia) na Maafisa wa UNHCR, leo wamesambaza misaada muhimu kwa familia zilizoathiriwa na mafuriko ya hivi majuzi huk…
UNRCO/ Fredbrannen Obadha
Naibu Rais Rigathi Gachagua (kushoto) akiandamana na ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa Kenya ukiongozwa na Mratibu Mkazi Dkt Stephen Jackson (kulia) na Maafisa wa UNHCR, leo wamesambaza misaada muhimu kwa familia zilizoathiriwa na mafuriko ya hivi majuzi huko Kiamaiko, Mathare, Kaunti ya Nairobi.

Vimbunga, mvua na mafuriko makubwa Afrika Mashariki UN itaendelea kusaidia

Tabianchi na mazingira

Umoja wa Mataifa unasema utaendelea kuunga mkono mamlaka za Afrika Mashariki dhidi ya madhila yanayotokana na mvua kubwa, mafuriko makubwa na vitisho vya vimbunga ambavyo vimesababisha mamia ya vifo na maelfu ya wengine kuyahama makazi yao.

 

Tweet URL

Ukanda huo unakabiliwa na mvua kubwa zaidi na mafuriko makubwa ambayo yameripotiwa kuua zaidi ya watu 350 tangu mwezi Machi mwaka huu.

“Mvua inaweza kuwa mbaya zaidi kutokana na kuwasili kwa kimbunga Hidaya, Shirika la Umoja wa Mataifa la Hali ya Hewa Duniani (WMO) limeonya jana Ijumaa Mei 3.

Tanzania

Msemaji wa WMO Clare Nullis amewaambia waandishi wa habari mjini Geneva hiyo jana Ijumaa kwamba kimbunga hiki cha kitropiki ni cha kwanza cha aina yake kutokea Afrika Mashariki na kitakuwa na "athari kubwa sana."

Kulingana na Nullis, hasa Tanzania itakabiliwa na madhara, kwani ardhi ina maji mengi na "inakaribia kupata mvua zaidi."

Kenya

Kenya pia iko katika hali ya tahadhari kufuatia bwawa la maji kufurika siku ya Jumatatu ya Aprili 29, na kusababisha vifo vya takriban watu 45.

Umoja wa Mataifa unaendelea kushirikiana na serikali na wadau kuwasaidia waathirika kama anavyofafanua Dkt. Stephen Jackson Mratibu Mkazi wa Umoja huo nchini Kenya.