Wakimbizi wa Darfur walioko CAR waanza kurejea nyumbani:UNHCR
Wakimbizi wa Sudan waliokuwa kwenye kambi za Bambari nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati CAR, wameanza kurejeshwa kwa hiyari nyumbani kufuatia uzinduzi wa zoezi hilo unaondeshwa na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR juma hili.