Kimbunga Mora chasambaratisha kambi za wakimbizi wa Rohingya
Kimbunga Mora kilichokuja na upepo mkali wa kilometa 117 kwa saa, kimepiga Kusini-Mashariki mwa Bangladesh Jumanne, na kuathiri mamia ya maelfu ya wakimbizi wa Rohingya katika kambi za Kutupalong na Nayapara, limesema Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi, UNHCR.