Vichwa vya Habari
Habari Moto Moto
Chaguo la Mhariri
Makala Maalum
Masuala ya UM
Je, itachukua nini kwa Palestina kuwa Nchi Mwanachama kamili wa Umoja wa Mataifa? Wakati Baraza la Usalama linashughulikia suala hilo wakati vita vya uharibifu huko Gaza vikiingia mwezi wake wa saba, tuliangalia hali ya sasa ya Palestina na kile kinachohitajika kuwa Nchi Mwanachama wa Umoja wa Mataifa.
Habari kwa Picha
Sudan: Hadithi za maumivu na mateso katika mwaka wa vita
Soha na Suhaila Ahmed, mwenye umri wa miaka 12, ni mapacha kutoka jiji la Nyala huko Darfur. Vita nchini Sudan viliwalazimu kutoroka pamoja na mama yao na mdogo wao hadi mji wa Port Sudan ulioko mashariki ya mbali ya Sudan, katika safari ngumu ya mabasi na malori ya mizigo, iliyochukua umbali wa kilomita 2,360. Wasichana hao wawili, mama yao mgonjwa, na mdogo wao wa kiume walipata makazi ya muda katika bweni la wanafunzi katika Chuo Kikuu cha Port Sudan, wakisubiri kurejea Khartoum baada ya vita kuisha. Wasichana hao wawili wanangojea hatima isiyojulikana. Nilishangazwa na nguvu na uvumilivu wa wasichana hawa wawili na kwamba bado waliweza kutabasamu na kuwa na matumaini baada ya kupitia uzoefu huo mgumu.
Habari Nyinginezo
Haki za binadamu
Kushindwa kwa Tanzania kulaani na kuchunguza mashambulizi dhidi ya watu wenye ualbino kunaweza kuwa ni ukiukwaji mkubwa wa wajibu wake wa kuwalinda watu wenye ulemavu, wamesema wataalamu wa Umoja wa Mataifa leo katika Ofisi za Umoja wa Mataifa mjini Geneva, Uswisi.
Amani na Usalama
Ripoti mpya ya kimataifa iliyotolewa leo na shirika la chakula na kilimo la Umoja wa Mataifa FAO kuhusu mgogoro wa chakula duniani inasema karibu watu milioni 282 walio katika nchi 59 walikabiliwa na viwango vya juu vya njaa mwaka 2023 ambayo ni sawa na mtu 1 kati ya 5 na sasa wanahitaji hatua za haraka kuepushwa na baa la njaa.