Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Geti la kuingia kwenye makao makuu ya ofisi ya haki za binadamu OHCHR mjini Geneva Uswis
UN Photo/Jean-Marc Ferré

OHCHR yakaribisha majuto ya ukiukwaji wa haki wa kihistoria Indonesia

Ofisi ya kamishina mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa OHCHR leo imesema"Tunakaribisha kukiri kwa Rais Joko Widodo wa Indonesia na kujieleza kwa majuto kuhusu matukio 12 ya kihistoria ya ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu, ikiwa ni pamoja na ukandamizaji wa kupinga Ukomunisti wa mwaka 1965-1966, mauaji ya waandamanaji mwaka 1982-1985, kutekelezwa kwa hatua za watu kutoweka mwaka 1997 na 1998, na tukio la Wamena Papua mwaka wa 2003. Ishara hii ya Rais ni hatua katika njia ndefu ya kuelekea upatikanaji wa haki kwa waathiriwa na wapendwa wao.” 

Kundi la wakimbiziwakishuka kutoka kwa boti lililokuwa limejaa maji baada ya kufika katika kisiwa cha Ugiriki cha Lesvos (30 Septemba 2015).
Photo: UNHCR/Achilleas Zavallis

Mashtaka yote dhidi ya wanaookoa wahamiaji baharini huko Ugiriki yafutwe- OHCHR

Umoja wa Mataifa umeelezea wasiwasi wake kuhusu kesi iliyoanza huko Lesvos nchini Ugiriki dhidi ya watetezi 24 wa haki za binadamu wanaoshtakiwa kwa kutekeleza jukumu la kuokoa wahamiaji ambao walikumbwa na zahma baharini wakati wakikimbilia barani Ulaya kusaka maisha bora. Kesi hiyo imeanza wiki hii baada ya kusubiriwa kwa muda mrefu.

Sauti
2'12"
Ukosefu wa usalama unazidi kushamiri nchini Haiti
JOA/Yes Communication Design

Uvunjaji wa sheria umetapakaa duniani, tuchukue hatua sasa- Katibu Mkuu UN

Hii leo Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limekuwa na mjadala wa wazi kuhusu utawala wa sheria ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa Matifa Antonio Guterres amesema ingawa nchi wanachama, mashirika ya kikanda, ya kiraia na sekta binafsi wana wajibu wa kuchangia katika kujenga na kulinda utawala wa sheria, hali ilivyo hivi sasa ni tofauti na kinachoonekana bado kuna safari ndefu ya kufikia lengo la utawala wa sheria.