OHCHR yakaribisha majuto ya ukiukwaji wa haki wa kihistoria Indonesia
Ofisi ya kamishina mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa OHCHR leo imesema"Tunakaribisha kukiri kwa Rais Joko Widodo wa Indonesia na kujieleza kwa majuto kuhusu matukio 12 ya kihistoria ya ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu, ikiwa ni pamoja na ukandamizaji wa kupinga Ukomunisti wa mwaka 1965-1966, mauaji ya waandamanaji mwaka 1982-1985, kutekelezwa kwa hatua za watu kutoweka mwaka 1997 na 1998, na tukio la Wamena Papua mwaka wa 2003. Ishara hii ya Rais ni hatua katika njia ndefu ya kuelekea upatikanaji wa haki kwa waathiriwa na wapendwa wao.”