Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Pichani iliyopigwa kutoka angani inaonyesha sehemu ya makazi kwenye kambi ya wakimbizi ya Kakuma nchini Kenya
Picha/Siegfried Modola

Kila mtu afahamu kuwa Kakuma kuna vipaji

Tamasha la kubaini vipaji lililofanyika kwenye kambi ya wakimbizi ya Kakuma nchini Kenya, likipatiwa jina “Kakuma’s Got Talent,” yaani ‘Kakuma ina vipaji’ limedhihirisha kuwa kuwa mkimbizi si kukosa kipaji ambapo wakimbizi vijana walionyesha vipaji mbalimbali ikiwemo kuimba, mitindo ya nguo na kucheza. 

Msafara wa wahamiaji wa Amerika ya kati ukipita Chiapas Mexico (2018)
IOM / Rafael Rodríguez

Uhamiaji uwe wa utu kwa kila mtu- IOM

Katika kuadhimisha siku ya uhamiaji duniani hii leo, Mkurugenzi Mkuu wa shirika la uhamiaji la Umoja wa Mataifa, IOM, António Vitorino ametaka hatua zaidi na za dharura zichukuliwe ili kulinda kundi hilo ambalo kila uchwao linakumbwa na madhila kote ulimwenguni.

Prise Josphine na Jemima Nsenga ni wakimbizi waliohamia nchi ya tatu Marekani, waliposhiriki hafla ya kukaribisha kupitishwa kwa mkata wa wakimbizi kwenye Umoja wa Mataifa.
UN News/Grece Kaneiya

Ukimbizi sio mwisho wa matumaini

Kuishi ukimbizini kuna changamoto kubwa lakini la msingi ni kukumbatia hali na kutia bidii kwa kila fursa uipatayo. Wito huo umetolewa na wasichana wawili wakimbizi ambao sasa wanaishi hapa Marekani baada ya kunufaika na mpango wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi , UNHCR wa kuwahamishia wakimbizi katika taifa la tatu. Wasichana hawa kabla ya kuja Marekani Prise Josephine mwenye umri wa miaka 16 raia wa Sudan aliishi kambini Kakuma Kenya kwa miaka 9 na Jemima Nsenga mwenye umri wa miaka 18  aliishi Uchina kama mkimbizi kwa miaka mitatu wamezungumza na Flora Nducha wa Idhaa hii