Hivi karibuni mjini Dar es Salaam, Tanzania kulifanyika Mkutano wa Kimataifa wa Idhaa za Kiswahili ambapo kulisailiwa taratibu za kuchukuliwa kipamoja kueneza matumizi sahihi, sanifu na fasaha ya lugha ili kujenga mazingira mapya ya utangazaji. Kongamano hili liliandaliwa na Baraza la Kiswahili Tanzania (BAKITA)na kuhudhuriwa na mashirika kadha ya redio na televisheni, ikiwemo pia Idhaa ya Redio ya Umoja wa Mataifa. Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa wa BAKITA, Suleiman Hegga, moja ya maazimio yaliopitishwa ni lile pendekezo linalotilia mkazo umuhimu wa kupunguza makosa ya utumiaji wa Kiswahili kisicho sahihi katika utangazaji, tatizo liliochipuka katika kipindi cha karibuni baada ya kukithiri kwa wadau wa lugha ya Kiswahili, ndani na nje ya Afrika ya Mashariki. Kwenye kipindi, tumeandaa mahojiano na Mwenyekiti Hegga ambaye anafafanua umuhimu wa idhaa zinazotumia Kiswahili kuimarisha matumizi ya Kiswahili sanifu.